Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge alia ukata balozi za Tanzania
Habari za Siasa

Mbunge alia ukata balozi za Tanzania

Mbunge wa Bunge la Tanzania, Felister Njau
Spread the love

 

MBUNGE wa Bunge la Tanzania, Felister Njau, ameeleza kusikitishwa na kitendo cha Serikali kushindwa kutoa fedha zinazopangwa kupelekwa kwenye balozi za Tanzania katika nchi mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mbunge huyo ameeleza hayo leo Ijumaa tarehe 17 Juni, 2022, wakati akichangia hoja ya bajeti ya Seriklai bungeni jijini Dodoma.

Njau amesema kuna balozi sita zilishindwa kutekeleza diplomasia ya uchumi kwa vitendoe kwa kutopelekwa kwa fedha zilizopangwa katika mwaka wa fedha 2020/21.

Amesema katika mwaka huo wa fedha Sh 116 milioni zilipangwa kupelekwa ubalozi wa Tanzania DRC lakini zilipelekwa 13 milioni sawa na asilimia 11.

Pia alisema ubalozi wa Lilongwe nchi Malawi ulitengewa Sh 57 milioni lakini zilizopelekwa ni Sh12 milioni, “tunaingiaje kwenye ushindani wa kiuchumi kama reception zetu hazipo vizuri,” amesema Njau.

Ameongeza kuwa ubalozi wa Ethiopia ulitengewa Sh138 milioni lakini zimepelekwa Sh2 milioni tu huku ubalozi wa Washington DC nchini Marekani ukitengewa Sh144 milioni lakini zilipelekwa Sh8 milioni tu sawa na asilimia saba, “how can we move kama nchi kama tunafanya mambo haya.”

Pia amesema watumishi wa balozi licha ya kubeba mzigo kwa kuwa pungufu lakini wamekuwa wakidai malimbikizo ikiwemo ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Malysia, DRC na Afrika Kusini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!