Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali: Tumedhibiti virusi vya Murburg
Afya

Serikali: Tumedhibiti virusi vya Murburg

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesema imefanikiwa kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya Murburg, huku ikiahidi kuutokomeza kwa kufuata miongozo ya Shirika la Afya Duniani (WHO). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne tarehe 4 Aprili 2023 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, akizungumzia mwenendo wa ugonjwa huo ulioibuka Machi mwaka huu, wilayani Bukoba, Mkoa wa Kagera.

“Napenda kusema kwamba, mlipuko huu ambao umeathiri sehemu ndogo ya Kagera, tunategemea kwamba tutaumaliza ndani ya siku chache kwa kuzingatia miongozo ya WHO,” amesema Mwalimu.

Mwalimu amesema, tangu ugonjwa huo uibuke hadi sasa, hakuna visa wala vifo vipya vilivyoripotiwa na kwamba idadi ya walioambukizwa imebaki kuwa nane ambapo kati yao, watano wamefariki dunia.

Waziri huyo wa afya amesema, mtu mmoja kati ya watatu waliolazwa kwa matibabu ya ugonjwa huo, ameruhusiwa huku akiitaka jamii inayomzunguka kutombagua kwa kuwa vipimo vimeonyesha hana virusi hivyo.

Amesema wagonjwa wawili wanaendelea na matibabu na kwamba hali zao kiafya zinazidi kuimarika.

Akizungumzia namna mwenendo wa ugonjwa huo ulivyodhibitiwa, Mwalimu amesema wizara yake kwa kushirikinaa na mamlaka mbalimbali nchini, ilifanikiwa kufuatilia watu 212 waliosaidika kukutana na waathirika ambapo watu 35 waliotangana nao moja kwa moja wamemaliza siku 21 za uangalizi na kubainika kwamba hawana dalili za ugonjwa huo.

Amesema, watu hao 35 wameruhusiwa kutoka katika karantini na kurejea katika familia zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!