Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kutoa ruzuku kwa halmashauri
Habari za Siasa

Serikali kutoa ruzuku kwa halmashauri

Mwita Waitara
Spread the love

SERIKALI imesema, inaendelea kutoa ruzuku ya maendeleo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuziwezesha kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo afya na elimu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 14 Mei 2019 bungeni na Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Leah Komanya (CCM).

Katika swali lake, Komanya alidai kwamba, moja ya kati ya vigezo vya ‘Capital Development Grant Assessment’ ni namna gani halmashauri inaweza kutoa taarifa kwa wananchi, juu ya mtiririko wa fedha ambazo serikali imepeleka katika halmashauri na miradi inayokusudiwa kutekelezwa.

“Je, kwanini mchakato huo ulisitishwa? Je, serikali haioni umuhimu wa kurejesha mchakato huo ambao utakuwa ukiongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya halmashauri nchini?” aliuliza Komanya.

Akijibu Waitara amesema, upimaji wa halmashauri ulikuwa ni kigezo cha kuziwezesha halmashauri kupata ruzuku ya maendeleo isiyo na masharti ‘Local Government Develeopment Grant’ kuanzia mwaka 2005.

“Miongoni mwa vigezo vilivyozingatiwa ni kuwepo kwa uwazi katika mapokezi na matumizi ya fedha kwenye ngazi za vijiji, kata na mitaa kwa kuhakikisha mapato na matumizi yanayobandikwa kwenye mbao za matangazo,” amesema.

Alisema serikali, inaendelea kutoa ruzuku ya maendeleo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuziwezesha kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali  zikiwemo afya na elimu.

“Wananchi wanachangia nguvu kazi na vifaa mbalimbali kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi hiyo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!