Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali kufufua mradi wa umwagiliaji ulioachwa na Mwalimu Nyerere
Habari Mchanganyiko

Serikali kufufua mradi wa umwagiliaji ulioachwa na Mwalimu Nyerere

Prof. Sospeter Muhongo, Mbunge wa Musoma Vijijini
Spread the love

 

SERIKALI imeamua kufufua mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Bwigema, Musoma Vijijini mkoani Mara, ulioasisiwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, kisha kukwama 1974. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, jana Jumapili, baada ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, kutoa tenda ya upembuzi yakinifu kuhusu mradi huo kwa Kampuni ya Ms Mhandisi Consultancy LTD.

Ofisi hiyo imesema kuwa, utekelezaji wa mradi umekuja baada ya Prof. Muhongo, kumuomba Rais Samia Suluhu Hassan, kuufufua ili kusaidia shughuli za kilimo na ufugaji zinazofanywa na wananchi.

“Rais Samia amepokea na kukubali ombi la kufufua kilimo cha umwagiliaji kwenye Bonde la Bugwema. Serikali iliyoongozwa na Mwalimu Nyerere ilianza kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwenye bonde hilo 1974, mradi ukasimama na sasa unafufuliwa,” imesema taarifa hiyo.

Akizungumza na wananchi kuhusu mradi huo, Prof. Muhongo amewataka washirikiane na Serikali katika utekelezaji wake ili ukamilike, huku akiwataka kuwapuuza watu wanaodai kwamba watahamishwa ili kuupisha.

“Serikali imeombwa kuwekeza Bonde la Bugwema na hii inataka iwe na utulivu hakuna atakayehamishwa. Kuna wajanja wanasema mtahamishwa, hamtahamishwa, waruhusu watalaamu wafanye tathimini ili baadae Serikali ipate miundombinu,” alisema Prof. Muhongo.

Kwa upande wa wananchi, wameishukuru Serikali kwa kuukumbuka mradi huo, wakisema ukikamilika utasaidia kuondoa changamoto ya ukame na kuwasaidia kulima kilimo cha biashara katika misimu yote.

Bonde la Bugwema lenye ukubwa wa hekta 10,000, linahudumia vijiji vitatu katika Jimbo la Musoma Vijijini, ikiwemo cha Masinono na Muhoji. Mazao yanayolimwa katika bonde hilo ni mpunga, mahindi, alizeti, dengu na pamba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!