Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serengeti kinara tena Afrika
Habari Mchanganyiko

Serengeti kinara tena Afrika

Serengeti
Spread the love

 

HIFADHI ya Taifa ya Serengeti iliyopo nchini Tanzania imeshinda tuzo ya kuwa hifadhi bora katika Bara la Afrika kwa mwaka 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa hifadhi hiyo ya Serengeti kushinda tuzo hiyo.

Tarifa iliyotolewa leo tarehe 21 Oktoba, 2021 na Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Pascal Shelutete imesema tuzo hiyo imetolewa na taasisi ya World Travel Awards (WTA) ya nchini Marekani ambayo ndiyo muandaaji wa tuzo hiyo kila mwaka.

Taarifa hiyo imesema kwa mara ya kwanza Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ilishinda tuzo hiyo ya kuwa hifadhi bora katika bara la Afrika mwaka 2019 na kwa mara ya pili ilikuwa mwaka 2020.

Hifadhi hiyo inayopatikana katika mikoa ya Arusha, Mwanza, Mara pamoja na Shinyanga, katika kipengelea hicho imezishinda hifadhi za Central Kalahari Game Reserve ya Botswana na Etosha Nationa Park ya Namibia.

Nyingine ni Kidepo Valley Nationa Park ya Uganda, Kruger National Park ya Afrika Kusini na Maasai Mara Nationa Rserve ya Kenya.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zaidi ya aina 70 za wanyama na aina 500 za ndege wanapatikana katika hifadhi hiyo iliyo na sifa ya kipekee duniani ikiwamo misitu na majani ya malisho ya wanyama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!