KAMPUNI ya Bia ya Serengeti Breweries Limited (SBL), imezindua kampeni yake ya ‘Maokoto chini ya Kizibo’ ambayo itawafanya wapenzi wa bia kuwa na kila sababu ya kutabasamu wakielekea benki, kutokana na kampeni kabambe ambayo itatoa zawadi zenye jumla ya kiasi cha Sh. 1.5 bilioni kwa muda wa miezi 3. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kampeni hiyo itakayowalenga wateja nchni kote, imezinduliwa jana katika ukumbi wa Kitambaa Cheupe Lounge, Sinza jijini Dar es Salaam na inatarajiwa kudumu mpaka mwezi Desemba, 2023. Kampeni hii inatoa fursa kwa kampuni kuwashukuru wateja wake na kuwataka kuendelea kufurahia bidhaa zake.
Kupitia hatua hii, SBL inalenga kuonyesha upendo na shukrani kwa wateja wake waaminifu huku ikiwataka kuendelea kufurahia bia yenye ubora wa hali ya juu. Katika wiki zijazo, SBL inakusudia kuwazawadia wateja wake na ofa za kusisimua, mashindano na zawadi, ikitoa fursa ya kushinda zawadi za kuvutia na kufurahia kumbukumbu za aina yake.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa East African Breweries Limited (EABL), Jane Karuku amesema, “Tunajivunia kutoa zawadi za kusisimua ambazo sio tu zitaleta furaha lakini pia kutoa frusa ya kujipatia kipato. Zawadi mbalimbali za kifedha zitanufaisha idadi kubwa ya wateja, hatimaye kuwasaidia watu wengi zaidi kuwa na kipato kwa muda mrefu.
Mkurugenzi Mtendaji wa SBL, Obinna Anyalebechi, amesisitiza, “MAOKOTO CHINI YA KIZIBO” inasukumwa na azma ya kuibua hisia za furaha na kusaidia maisha ya wateja wetu, na nia ya kuacha alama muhimu kwa kuleta sababu za kusherekea kila mahali, na kujitolea kwetu kwa namna ya kipekee kusaidia jamii yetu.”
Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa SBL, Anitha Rwehumbiza, ameongezea kuwa kampeni hiyo itafanyika kwa muda wa miezi mitatu wakiwa wameandaa zawadi zenye thamani ya TZS Bilioni 1.5. Amesema, “Tutakuwa tunatoa zawadi za TZS 4M kila wiki na zawadi nyinginezo za papo kwa hapo kila watakapokuwa wananunua bidhaa zetu mbalimbali kama vile Serengeti Premium Lite, Serengeti Premium Lager, Pilsner, Guiness Smooth, na Smirnoff Ice Black”.
William Lyimo, a.k.a. BillNass, mwanamuziki mashuhuri katika Tasnia ya burudani Tanzania na balozi wa kampeni hiyo, amesema, “Nimefurahia dhamira ya SBL katika kuleta furaha na kusaidia maisha ya wateja wake. ‘MAOKOTO CHINI YA KIZIBO’ inaburudisha, hata kwa masharti yake, tayari unaweza kujionea namna ilivyopokelewa vizuri sokoni”.
Namna ya kupata maokoto
Mbona hakuna zawadi na tunakunywa Serengeti lite kama zote,ila 2013 kwa kweli mlitisha zawadi zilikuwa kama zote
Hello
Mbona nimejaza code mpaka bac lkn sioni lolote
Maokoto chini ya kizibo inachezwaje. Unapoulizwa weka code maana yake nini, na unatakiwa code gani ?
Inachezwaje jamani naomba msaada
Yaani hii nimeijua leo wakati nakunywa mara naangalia chupa kusoma katangazo ukishalewa kama kawaida yetu wanywaji naona maokoto. Nimeingiza vizibo 6, 2 kati yake vimenipa zawadi ya sh 500 kila kimoja.
Nimefulai mno kusikia uwepo wa s b l maokoto kama kawa uku mtaani mpaka sasa nipo kwenye droo mimi😎
Namba za kutuma herufi
Nimetuma sanaa mbona sijabata zawadi hizo
Jinsi ya kucheza …?
Nacheza sbl maokoto kwa namba 0622991175 nashinda ila sioni pesa ila namba hii ni ya wakala 515583 inaweza kuwa sababu
Ninakunywa Serengeti lite beer na vizibo kwa ndani vina herufi.je Kuna jinsi ya kutuma au zawadi zinapatikana ndani ya vizibo.naomba kuelimishwa jinsi ya kupata zawadi
Maelekezo yapo kwenye Chupa ya Bia unayokunywa.
Bonyeza simu yako *150*80# kisha weka namba zilizopo upande wa ndani ya kizibo na tuma. Utakuwa umekwisha shiriki draw za Maokoto. Zawadi zingine papo hapo kwenye kizibo pia zipo kama tulivyoambiwa. Kazi kwetu.
Tunaomba maelekezo jinsi ya kucheza?
nmeshinda sana jero jero
Mi wakunywa Serengeti Tisa na kupata hero kweli😂
Kwa mm sijapata zawadi yeyote kuanzia nimeanza kucheza MAOKOTO CHINI YA KIZIBO
Ndiyo nn hy?
Tunaingiza code mwanzoni tu tunapata hizo 500 lakini badae naweka code mnatuma sms kwamba nimeingia kwenye droo nimeshinda 500 lakini hela hamtumi kwenye muamala naomba mliangalie hilo zaidi ya kreti 2 za serengeti lite tumekunywa lakini visoda vilivyokubali ni 7 tu
Unyama ni mwingi naendelea kuokota pesa za vocha,
Yaani ni HATARI SANA NI BALAA SANA ukiwa na Serengeti lite mkononi.
Ukiona hupati bhasi me nakuonea wivu kwasababu wewe utakuja kupata babukubwa zaidi so msikate tamaaa endeleeni kuhuda Serengeti lite. USHINDI UPO JAMANI OHOOOOO WE KATA TAMAA SISI TUENDELEE KUCHEZA NA VIZIBO KAMA KINDAGATEN PUPILS 🤣🤣🤣🫵🫵🫵🫵🙏
SBL ipo sawa kabisa ladha ya kijanja
Nachezaje nko baa now
Inafanya kazi nimejaribu vizibo 3 nimepata kimoja
Hii ni batili i have drank more than 100 beers didn’t get anything
Jamani nawapongeza,Hira mbona mimi nimejaza cete zaidi ya 50,Lakini iliyo kubali ni moja tu.
Nimeshinda Tshs 500/= mara 4 kwa nyakati tofauti, jumla Tshs 2000/= je nazipataje?