Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Samia ashuhudia utiaji saini mikata 26 ya trilioni 1.9
Habari Mchanganyiko

Samia ashuhudia utiaji saini mikata 26 ya trilioni 1.9

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan leo Jumanne ameshuhudia utiaji saini mikataba 26 yenye thamani ya Sh trilioni 1.9 ambayo itakwenda kuimarisha upatikanaji wa umeme kwenye mfumo wa gridi ya Taifa katika mikoa mbalimbali Tanzania Bara.

Awamu ya kwanza ya mradi huo unaotekelezwa kwa muda wa miaka minne katika muda wa mwaka mmoja utagharimu Sh bilioni 500. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya wizara ya nishari kwa kushirikiana na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kufanya tathmini na ukaguzi kuhusu chanzo cha kukatika kwa umeme na kubaini kuwa kuna ongezeko la matumizi makubwa ya umeme.

Mbali na ongezeko hilo pia matumizi ya mitambo chakavu isiyotosheleza na isiyo na usanifu bora kuweza kukidhi mahitaji ya umeme na shughuli za kiuchumi, ndio chanzo cha tatizo hilo.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Samia Suluhu Hassan amesema bado kuna kazi kubwa ya kufanya katika kufikisha umeme katika vitongoji vyote nchini hasa ikizingatiwa sasa ni asilimia 43.9 pekee ya vitongoji hivyo vimefikiwa na huduma ya umeme.

Akifafanua namna mchakato wa mradi huo wa gridi imara ulivyoanza, Rais Samia amesema awali Waziri wa Nishati, Januri Makamba alimpeleka bajeti ya Sh trilioni 11 na kumrudisha.

Amesema baada ya kuridhia marekebisho ambayo wizara iliyafanya kulingana na upatikanaji wa fedha, maboresho hayo ya gridi ya Taifa yanalenga kuboresha upatikanaji wa umeme kwenye migodi hasa ya wachimbaji wadogo, vituo vya afya pamoja na skimu za umwagiliaji ambazo zinahitaji umeme kusukuma maji kuelekea kwenye mashamba ya vijana wanaoshiriki mpango maalumu wa serikali kuimrisha kilimo biashara.

“Miradi hii itapeleka maeneo 336 ya uzalishaji mali nchini, itatusaidia kujenga uchumi kwani vitongoji 1522 vitapata umeme pamoja na vituo vya afya hasa ikizingatiwa nchi yetu ni kubwa lakini hatua kwa hatua tutamaliza mradi huu licha ya kwamba tunajua malalamiko yatakuwepo lakini tutakwenda hadi tumalize,” amesema.

Aidha, Samia ameonya kuwa ili miradi hiyo ifanyike kwa haraka kwa kuzingatia maamuzi ya haraka.

Ameonya wakandarasi waliokosa zabuni za utekelezaji wa miradi hiyo kutokwenda kukata rufaa kwa mujibu wa sheria kwani watachelewesha utekelezaji wa miradi kwa sababu anaamini wakandarasi waliopitishwa ndio wakandarasi stahiki.

Pia amezitaka taasisi husika kama vila Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kutozuia miradi hiyo kufanyika kwa haraka.

“Niwaombe sana pimeni yanayoletwa kwenu, msiturudishe nyuma kwa sababu sheria inaruhusu kufanya hivyo ndani ya miezi mitatu, kama waliowapitisha wakandarasi hawa kwa kuchukua rushwa, mkandarasi akivurunda mimi na wao,” amesema.

Pia amezitaka taasisi za serikali zinazohusika na utoaji wa vibali vya ajira kwa ajili ya wafanyakazi wa miradi hiyo, zisiweke urasimu kama uliotokea kwenye Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambayo ilitumia mwaka mzima kuomba vibali ilihali suala la ukusanyaji wa kodi ni muhimu.

Pamoja na kupongeza kwa watanzania kupata kandarasi kwenye miradi hiyo, amewaonya kutotafuna fedha na kuanza kugawa kazi kwa wengine ili kupunguza gharama za kazi.

Ameionya pia wizara ya fedha kuhakikisha inatoa fedha za malipo kwa wakati pindi mkandarasi anapokamilisha kazi yake badala ya kuwazungusha ili wakandarasi wazawa wakue.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!