Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia amlilia Rais Namibia
Habari za SiasaTangulizi

Samia amlilia Rais Namibia

Spread the love

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameeleza kusikitishwa na kifo cha Rais wa Jamhuri ya Namibia, Dk. Hage Gottfried Geingob kilichotokea leo Jumapili jijini Windhoek nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Jumapill na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imesema Rais Samia amekuwa na urafiki wa muda mrefu na Dk. Geingob ambaye alikuwa anamuita kaka.


Rais Samia ametuma salamu za rambirambi kwa niaba ya Watanzania kwa wananchi wa
Namibia, serikali ya nchi hiyo pamoja na mke wa marehemu, Monica Geingob, na familia kwa ujumla.

“Nimesikitishwa sana na msiba wa kaka yangu Rais wa Namibia, Dk. Geingob, ambaye nimemfahamu kuwa kiongozi msikivu, mtu wa watu na amekuwa miongoni mwa alama za ukombozi wa Namibia,” Rais Samia amesema.

Kufuatia undugu na urafiki wa muda mrefu na Namibia, Rais Samia pia ametoa pole kwa uongozi na wanachama wote wa chama tawala rafiki cha SWAPO.

Mara ya mwisho Rais Samia alipokelewa kwa ukarimu mkubwa na Rais Geingob nchini Namibia tarehe 7 Mei 2023 alipokwenda kuhudhuria mkutano wa dharura wa utatu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Troika).

Viongozi hao wawili walizungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili, hususan kisiasa na kiuchumi.

Tanzania na Namibia zimekuwa na uhusiano wa kindugu na wa muda mrefu tangu wakati wa harakati za ukombozi wa Taifa hilo.

“Aidha, uhusiano umeendelea kuimarika zaidi siku hadi siku. Mungu ailaze roho ya Rais Dkt. Hage Gottfried Geingob mahali pema peponi, Amin,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!