Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limetangaza kuendelea kufanya uchunguzl wa tuklo la mauaji ya Mkuu wa kituo kidogo cha Polisi Chiungutwa Wilaya ya Masasi, Eliuterius Eliuterius Hyera aliyefariki dunia tarehe 1 Februari mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Hyera alifariki wakati akiwa anaendelea kupatowa matibabu katika Hospitali ya Ndanda wilayani Masasi mkoani Mtwara baada ya kujeruhiwa kwa risasi.
Taarifa iliyotolewa leo tarehe Jumapili na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara ACP Nicodemus Katembo imeeleza kuwa katika siku hiyo ya tarehe 1 Februari, Hyera alijeruhiwa kwa risasi akiwa ameongozana na askari mwenzake katika ukamatajl wa mtuhumiwa wa tukio la kuvunja oflsi na kulba.
“Mtuhumlwa huyo alianza kukimbia ill asikamatwe ndipo askari aliyekuwa na bastola alipofyatua risasi kwa lengo la kufanikisha ukamataji na ikapelekea kumjeruhi Mkaguzi huyo.
“Juhudi za kuokoa maisha yake illfanyika kwa kupelekwa Hospitall ya Ndanda ambapo alifariki dunia akiendelea na matibabu,” ameeleza Kamanda huyo.
Amesema mwill wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Ndanda kwa uchunguzi zaldi na mtuhumiwa anashikiliwa kwa hatua zaidi za kisheria.
Aidha, amesema juhudi za kuwasaka watu waliohuslka katika tukio hilo na kuvunja na kuiba, zinaendelea kufanylka ili kuwafikisha mbele ya sheria.
Leave a comment