Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Safari ya mwisho ya Hayati Magufuli Chato
Habari MchanganyikoTangulizi

Safari ya mwisho ya Hayati Magufuli Chato

Jeneza lililobeba mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli
Spread the love

 

MWILI wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli unazikwa leo Ijumaa tarehe 26 Machi 2021, katika makaburi ya nyumbani kwao, Chato mkoani Geita.

Viongozi mbalimbali wamehudhulia katika shughuli hiyo ya mwisho ya Hayati Magufuli inaanzisa Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Magufuli, wakiongozwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Dk. Magufuli, alifariki dunia Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, kwa ugonjwa wa mfumo wa umeme wa moyo.

Baadhi ya viongozi waliopo uwanjani hapo kunakofanyika misa takatifu kukifuatiwa na salamu mbalimbali ni; Marais wastaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete, Ali Hassan Mwinyi.

Wengine ni, Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othuman Masoud Othuman na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!