Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Maaskofu 15, Mapadri 70 wamzika Magufuli
Habari Mchanganyiko

Maaskofu 15, Mapadri 70 wamzika Magufuli

Spread the love

 

MAASKOFU 15 na mapadri zaidi ya 70 wa Kanisa Katoliki, wanashiriki misa takatifu ya kumwombea Hayati John Pombe Joseph Magufuli. Anaripoti Regina Mkonde, Chato …(endelea)

Misa takatifu inafanyika Uwanja wa Mpira wa Magufuli, Chato mkoani Geita leo Ijumaa, tarehe 26 Machi 2021.

Misa hiyo inaongozwa na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanania (TEC), Gervas Nyaisonga.

Baada ya kumazilika kwa misa hiyo, kutafutia salamu za viongozi mbalimbali akiwemo Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kisha safari ya kwenda makaburi ya familia itaanza ili kuuzika mwili huo.

Misa ya maziko, itaongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge-Ngara, Severine Niwemugizi.

Dk. Magufuli, aliyekuwa Rais wa Tanzania, alifariki dunia Jumatano tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu kwa habari na taarifa mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!