ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoani Kilimajaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne, leo Ijumaa, tarehe 4 Juni 2021, wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea)
Sabaya amekuwa akishikiliwa kwa zaidi ya 10 kwa mahojiano na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa tuhuma mbalimbali zinazomkabili za matumizi mabaya ya madaraka.
Uchunguzi huo, umefanyika baada ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kumsimamisha hivi karibuni ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu kwa habari na taarifa mbalimbali
Leave a comment