Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mfumo wa elimu Tanzania kujadiliwa
Elimu

Mfumo wa elimu Tanzania kujadiliwa

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga
Spread the love

 

HUSNA Sekiboko, mbunge wa viti maalum, aiomba Serikali ya Tanzania, kufanya marekebisho ya mtaala wa elimu ya msingi na sekondari. Anaripoti Jemima Samwel DMC … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa, leo Ijumaa, tarehe 4 Juni 2021, katika kipindi cha maswali na majibu bungeni jijini Dodoma.

Sekiboko amesema, Serikali inapaswa kutambua umuhimu wa kufanya marekebisho ya mtaala ya ngazi hiyo ili kuendana na uhitaji wa sasa.

“Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ya malengo ya mtaala wa elimu ya Msingi na Sekondari nchini ili kuendana na uhitaji wa sasa?”

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Juma Kipanga amesema, Serikali inatambua umuhimu wa kufanyia marekebisho Mitaala ya Elimu ya Msingi na Sekondari ili kuwawezesha wanafunzi kupata stadi mbalimbali zinazoendana na mahitaji ya wakati.

“Kwa sababu hiyo, Serikali imekuwa ikiboresha mitaala hiyo kila kunapokuwa na hitaji la kisayansi, kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kiteknolojia.”

“Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imepanga kufanya mjadala mpana kuhusumfumo wa Elimu nchini ambao utahusisha Sera ya elimu na mitaala kwa ujumla ili iendane na wakati na ikidhi mahitaji ya sasa na baadae,” amesema Kipanga.

Kipanga amesema, katika mjadala huo mpata “tutakwenda kuudadavua na kuuweka kwenye mawanda mapana” ili malengo ambayo wadau mbalimbali wa elimu wanataka, yanakwenda kufanyiwa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!