Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Risasi zakosesha soko ng’ombe wa Loliondo
Habari Mchanganyiko

Risasi zakosesha soko ng’ombe wa Loliondo

Spread the love

BAADHI ya ng’ombe katika kijiji cha Arash Loliondo, Ngorongoro, mkoani Arusha, wameshindwa kupata soko kutokana na kuwa na majeraha ya risasi huku wengine wakiendelea kuishi na risasi hizo mwilini, anaandika Nasra Abdallah.

Ng’ombe hao walipigwa risasi wakati wa operesheni ya kuwaondoa mifugo iliyofanywa na Mamlaka  za Hifadhi kwa lengo la kutaka kumega eneo la kilometa 1500 katika vijiji vinavyozunguka hifadhi ya Serengeti na kupafanya pori tengefu.

Timu ya waandishi ambayo ilifika katika vijiji vilivyoathiriwa na zoezi hilo kwa lengo la kujionea athari za kiuchumi zilizotokana na operesheni hiyo, ilielezwa kwamba kwa sasa kumekuwa na umasikini wa hali ya juu kutokana na ukweli kwamba uchumi mkubwa wanaoutegemea wakazi wa maeneo hayo ni mifugo.

Mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Ngostelo Lilash, amesema awali kabla ya operesheni waliweza kuuza ng’ombe mmoja hadi Sh. milioni moja, lakini kutokana na mifugo hiyo kwa sasa kuwa na majeraha ya risasi na wengine kuwa wadhoofu kutokana na ukame wameshuka bei  hadi Sh. 400,000.

Naye Kutare Kumari, amesema wamekuwa wakilazimika kumlipa daktari kwa kutibu ng’ombe mmoja kwa Sh. 50,000 kila siku na hivyo ng’ombe mmoja kuwagharimu Sh. 350,000 kwa wiki.

Kama vile haitoshi amesema mpaka sasa wananuka madeni ya kukopa kwa riba  ili kuweza kiwakomboa ng’ombe wao waliokamatwa kipindi cha operesheni hali inayowafanya maisha yao kuzidi kuwa magumu.

“Mbali na kukopa fedha pia tunalazimika wakati mwingine kuuza kondoo kwa hasara ili  kuweza kukomboa ng’ombe wetu ambapo mpaka sasa timeshatumia zaidi ya milioni kumi katika shughuli hiyo na bado tunadaiwa fedha,” amesema Kumari.

Wito  wao kwa serikali, wakazi hao waliomba serikali iwape mifugo yao kwa kuwa ilikamatwa nje ya hifadhi na kuongeza kuwa ni vema idara ya mifugo katika Halamshauri ya Ngorongoro kuwapelekea madaktari wa mifugo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!