Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Rekodi ya 1977 inayosakwa na wachezaji Simba, Yanga
Michezo

Rekodi ya 1977 inayosakwa na wachezaji Simba, Yanga

Spread the love

 

WACHEZAJI wa kabu kubwa Tanzania – Simba na Yanga zote za jijini Dar es Salaam, wana jambo ambalo hawajaweza kulifanya tangu lilipofanyika mwaka 1977. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Jambo hilo ni rekodi ya hat-trick iliyofanywa na mchezaji wa zamani wa Simba, Abdallah Kibadeni ‘King Kibaden’ tarehe 19 Julai 1977, dhidi ya hasimu wao Yanga.

Katika mchezo huo, Kibadeni aliifunga Yanga bao tatu kuanzia dakika ya za 10, 42 na 89 ambapo mchezo huo ulimalizika kwa Yanga kufungwa bao 6-0.

Selemani Matola, Kocha Msaidizi wa Simba

Magoli mengine yalifungwa na Suleiman Sanga, beki wa Yanga aliyejifungwa mwenyewe ambapo magoli mawili yalifungwa na Jumanne Hassan.

Tangu mwaka huo, hakuna mchezaji yeyote aliyewahi kufunga bao tatu katika mechi zinazokutanisha watani hao wa jadi.

Mpaka sasa, rekodi zinaonesha Simba na Yanga zimekutana mara 105, ambapo Yanga ameshinda mara 37, Simba 31 sare zikiwa 37.

Kocha Mkuu wa Yanga, Nadreddine Al Nabi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!