WACHEZAJI wa kabu kubwa Tanzania – Simba na Yanga zote za jijini Dar es Salaam, wana jambo ambalo hawajaweza kulifanya tangu lilipofanyika mwaka 1977. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Jambo hilo ni rekodi ya hat-trick iliyofanywa na mchezaji wa zamani wa Simba, Abdallah Kibadeni ‘King Kibaden’ tarehe 19 Julai 1977, dhidi ya hasimu wao Yanga.
Katika mchezo huo, Kibadeni aliifunga Yanga bao tatu kuanzia dakika ya za 10, 42 na 89 ambapo mchezo huo ulimalizika kwa Yanga kufungwa bao 6-0.

Magoli mengine yalifungwa na Suleiman Sanga, beki wa Yanga aliyejifungwa mwenyewe ambapo magoli mawili yalifungwa na Jumanne Hassan.
Tangu mwaka huo, hakuna mchezaji yeyote aliyewahi kufunga bao tatu katika mechi zinazokutanisha watani hao wa jadi.
Mpaka sasa, rekodi zinaonesha Simba na Yanga zimekutana mara 105, ambapo Yanga ameshinda mara 37, Simba 31 sare zikiwa 37.

Leave a comment