Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa
ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the love

Mkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na mienendo ya kesi zinazowahusu watu wanaodaiwa kuwapa ujauzito wanafunzi na kukatisha masomo yao, kwenda kwa kusuasua na kusisitiza adhabu zaidi itolewe kukomesha ‘mafataki’ hao. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea).

Dk. Michael aliyasema hayo jana Jumatano kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC) mkoani humo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wadau wa taasisi mbalimbali.

Alisema serikali imetumia fedha nyingi kujenga shule ili watoto wasome na wawe viongozi wa baadae, lakini wapo vijana wanaojiita mabeberu wanaharibu na kukatisha ndoto za wanafunzi hao kwa kuwarubuni na kufanikiwa kuwapa ujauzito.

Mkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael akizungumza na wajumbe kwenye kikao cha RCC mkoani humo.

Alisema takwimu alizonazo ni kuwa watoto 60 waliopewa ujauzito, kesi zao zilipelekwa mahakamani lakini ni kesi mbili pekee zilizotolewa hukumu huku nyingine zikiwa hazijulikani hatma yake.

Alisema kutokana na kasi ya serikali kujenga, madarasa mapya na kuanzisha shule mpya sambamba na ujenzi wa mabweni ipo haja wadau kushirikiana kuwalinda watoto ili wasome shule bila kusumbuliwa na itolewe adhabu kali kwa mtu atakayebainika anamrubuni mtoto wa kike.

Aidha, Dk. Michael aliwaeleza wadau wakiwemo wabunge kujenga utamaduni wa kuwasomesha watoto wenye uhitaji maalum wakiwemo yatima ili waweze kumaliza masomo yao na kujiendeleza kimaisha kwani Mungu atawaoa thawabu kubwa.

Naye Mbunge wa Songwe, Philipo Mulugo (CCM) alisema tangu awe mbunge kwa zaidi ya miaka 10, amesomesha watoto 720 huku Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM) akisema anasomesha watoto 60.

Matukio ya mimba za utotoni katika mkoa wa Songwe yamefikia asilimia 45 kitaifa na kuufanya mkoa huo ya kuongoza kwa matukio hayo yanayokatisha ndoto za wasichana kusoma

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!