Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko RC Shigela awaonya maofisa ugani wasiokuwa na mashamba darasa
Habari Mchanganyiko

RC Shigela awaonya maofisa ugani wasiokuwa na mashamba darasa

Spread the love

 

MKUU wa mkoa wa Morogoro, Martin Shigela amewata maofisa ugani kutumia taaluma yao kivitendo kwa kuweka mashamba darasa na kuwapa elimu wakulima itakayoleta tija ya kilimo katika maeneo yao. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Hayo yalisemwa na Mkuu wa wilaya ya Malinyi, Mathayo Masele k,wa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro, wakati akizindua kituo mahili cha usambazaji wa teknolojia za kisasa za kilimo mkoani humo, kilichoandaliwa na Taasisi ya utafiti wa Kilimo nchini (TARI) kikiwa na wataalamu wa mafunzo kwa wakulima  ili kuongeza tija na uzalishaji.

Masele alisema zipo wilaya nyingi ambazo zina maafisa ugani ambao wakiulizwa kazi wanazofanya na kutakiwa kuonesha mashamba darasa yao yalipo hukosa vya kujieleza.

“Kama kuna Afisa ugani anajijua hana shamba darasa na bado anaipenda kazi yake, abadilike mara moja” alisema.

 

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kituo hicho mkurugenzi Mkuu wa TARI, Dk. Geofrey Mkamilo alisema kituo hicho kitakachotoa mafunzo mwaka mzima kitakuwa na wataalamu mbalimbali wa kilimo wakiwemo watafiti na wataalamu wa huduma za ugani watakaotoa elimu ya mazao mbalinbali kwa wakulima.

Dk. Mkamilo alisema TARI iko tayari kuhakikisha inaleta mapinduzi ya kilimo na kuhamasisha wakulima kuachana na kilimo mazoea walichokuwa wanalima mababu na mabibi.

Alisema katika kuboresha kilimo na kuongeza uzalishaji nchini TARI imekuwa ikifanya kazi na taasisi nyingine ikiwemo taasisi ya udhibiti wa ubora wa mbegu TOSCI, wakala wa mbegu ASA, na makampuni mengine ya uzalishaji na usambaza mbegu ili kumfanya mkulima kupata elimu ya kilimo na kujua mbegu zinapatikana wapi.

Dk. Mkamilo alisema TARI inaratibu shughuli za utafiti na kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kilimo na ubunifu kwa lengo la kuongeza tija ya kilimo nchini.

Naye Mkurugenzi wa kituo cha utafiti TARI Mlingano-Tanga, Dk. Catherine Senkolo aliwashauri wakulima wa migomba kulima mazao ya mikundekumbe kwenye shamba la migomba ili kutunza unyevunyevu na pia kutengeneza mbolea ya samadi.

Dk. Senkolo alisema mikundekunde kwenye shamba la migomba pia linasaidia kuondoa ugonjwa wa minyoo kwenye migomba ambao umekuwa ukisababisha uzalishaji kupungua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yatoa msaada wa mil. 20 kwa waathirika mafuriko Hanang

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) sambamba na wafanyakazi wa...

Habari Mchanganyiko

Polisi wadaka mirungi kwenye basi la Extra Luxury

Spread the loveJeshi la polisi mkoani Kilimanjaro limekamata shehena ya dawa za...

Habari Mchanganyiko

Oryx yaungana na jamii kuwafariji waathirika maporomoko Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeungana na Watanzania kutoa pole...

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

error: Content is protected !!