Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Kunenge atangaza fursa za biashara Dar
Habari za Siasa

RC Kunenge atangaza fursa za biashara Dar

Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Aboubakar Kunenge amewataka wafanyabishara kuchangamkia fursa ya baishara katika Kituo cha Kimataifa cha Mabasi Mbezi Lius jijini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kituo hicho kitakachokuwa kikuhudumia mabasi ya mikoani na yanayokwenda nje ya mipata ya Tanzania, ujenzi wake umefikia asilimia 90.

RC Kunenge amesema hayo leo Jumatatu tarehe 9 Novemba 2020 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema, majaribio ya kituo hicho itakuwa tarehe 25 Novemba 2020 na kutumika rasmi 30 Novemba.

Mkuu huyo wa mkoa, ametoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara kuchangamkia fursa zinazopatikana kwenye kituo hicho ikiwemo fremu za maduka, migahawa, ofisi, huduma za kifedha, supermarket, ofisi za kukata tiketi na hotel.

Kunenge amewataka wananchi wanaohitaji maeneo kutuma maombi kuanzia leo Jumatatu hadi tarehe 25 Novemba 2020.

Amesema, uwepo wa kituo hicho kitaendelea kufungua fursa za maendeleo kwa wakazi wa Ubungo hivyo amewataka kujiandaa kwa hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!