Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia: Tunawagonjwa wa corona zaidi 100
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia: Tunawagonjwa wa corona zaidi 100

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, zaidi ya wagonjwa 100 wa maambukizi corona (COVID-19), wamebainika nchini humo na wanaendelea na matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Amesema, kati ya wagonjwa 70 wanaendelea na matibabu ya gesi ili kuhakikisha wanapona.

Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu, tarehe 28 Juni 2021, Ikulu ya Dar es Salaam, wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa habari, kuhusu siku 100 za utawala wake tangu alipoingia madarakani.

Alikuwa akijibu swali aliloulizwa juu ya mikakati ya makusudi ya kupambana na ugonjwa huo.

“Nilipoingia madarakani nilitamani tushughulike na corona kama inavyoshughulikiwa duniani. Niliunda kamati ya wataalamu, wakafanya na kuleta ripoti na tumeamua kwenda kama dunia inavyokwenda.”

“Mpaka juzi Tanzania kuna wagonjwa wa corona kama miamoja na, na kati yao 70 wako kwenye matibabu ya gesi kama takwimu za juzi. Tunapaswa kujikinga wasiongezeke,” amesema Rais Samia

Kuhusu chanjo, Rais Samia amesema “chanjo ya corona itakuja Tanzania lakini itakuwa hiari kwa mtu kuchanjwa, haitakuwa lazima.”

Ameendelea kuwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari ya maambukizi hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!