RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, zaidi ya wagonjwa 100 wa maambukizi corona (COVID-19), wamebainika nchini humo na wanaendelea na matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Amesema, kati ya wagonjwa 70 wanaendelea na matibabu ya gesi ili kuhakikisha wanapona.
Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu, tarehe 28 Juni 2021, Ikulu ya Dar es Salaam, wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa habari, kuhusu siku 100 za utawala wake tangu alipoingia madarakani.
Alikuwa akijibu swali aliloulizwa juu ya mikakati ya makusudi ya kupambana na ugonjwa huo.
“Nilipoingia madarakani nilitamani tushughulike na corona kama inavyoshughulikiwa duniani. Niliunda kamati ya wataalamu, wakafanya na kuleta ripoti na tumeamua kwenda kama dunia inavyokwenda.”
“Mpaka juzi Tanzania kuna wagonjwa wa corona kama miamoja na, na kati yao 70 wako kwenye matibabu ya gesi kama takwimu za juzi. Tunapaswa kujikinga wasiongezeke,” amesema Rais Samia
Kuhusu chanjo, Rais Samia amesema “chanjo ya corona itakuja Tanzania lakini itakuwa hiari kwa mtu kuchanjwa, haitakuwa lazima.”
Ameendelea kuwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari ya maambukizi hayo.
Leave a comment