Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia kuhutubia taifa leo
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kuhutubia taifa leo

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

LEO Jumatano tarehe 8 Desemba 2021, saa 3:00 usiku, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, atalihutubia taifa kupitia vyombo mbalimbali vya habari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hii itakuwa hotuba yake ya kwanza kwa vyombo vya habari kuitoa, tangu aingie madarakani tarehe 19 Machi 2021, akichukua nafasi iliyoachwa na Rais John Pombe Magufuli, aliyefariki dunia.

Rais Magufuli, alifariki dunia jioni ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, iliyopo Makumbusho jijini Dar es Salaam na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwao, Chato mkoani Geita.

Rais Samia atatoa hotuba hiyo ikiwa zimesalia saa chache, kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara, uliopatikana 9 Desemba 1961 kutoka kwa Wakoloni.

Kilele cha sherehe hizo itakuwa kesho Alhamisi, katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na Rais Samia, atakuwa mgeni rasmi.

Channeli yetu ya mtandaoni ya MwanaHALISI TV itakuletea moja kwa moja hotuba hiyo huku mitandao yetu ya kijamii itakuwa ikiripoti hotuba hiyo.

MwanaHALISI TV itakuletea matangazo hayo moja kwa moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!