SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania ameipongeza timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 (U23), kwa kutwaa ubingwa wa mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA-2021). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Timu hiyo ilitwaa ubingwa huo tarehe 30 Julai 2021, nchini Ethiopia kulikofanyika michuano hiyo kwa kuwafunga kwa penati vijana wenzao kutoka Burundi kwa 6-5.
Ni baada ya dakika 90 kumalizika kwa kutokufungana.
Leo Jumapili, tarehe 1 Agosti 2021, timu hiyo imerejea nchini na kupokelewa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallece Karia, ameipokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Nawapongeza timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 23 kwa kutwaa ubingwa wa Mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA-2021). Ushindi huu ni heshima kwa nchi yetu na ni chachu ya kukuza michezo. Natoa wito kwa wadau wa michezo kuendeleza jitihada za kukuza michezo yetu. pic.twitter.com/tSLJiTb6Gv
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) August 1, 2021
Rais Samia ametoa pongezi hizo kupitia ukara wake wa kijamii wa twitter akisema “Nawapongeza timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 23 kwa kutwaa ubingwa wa Mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA-2021).”
“Ushindi huu ni heshima kwa nchi yetu na ni chachu ya kukuza michezo. Natoa wito kwa wadau wa michezo kuendeleza jitihada za kukuza michezo yetu,” amesema
Vijana hawa.wametuletea heahina kubwa sana Tanzania lakini pia inaonesha moira wetu umetua. Under 23 ni kama Timu ya Taifa maana miaka 23 ni utu uzima.katika mi
hezo. Mchezaji akifikia umri wa miaka26 Amanda kuzeeka Kimchezo, sasa hawa under 23 ndio wenyewe.wa Taifa kuanzia.2022
. Ningekuwa mdau mkubwa kama kina Manji, Mo, GSM n.k ningewazawadia Tshs 10 millioni kila mchezaji, na viongozi.wa Timu Tshs. 20 millioni kila mmoja, Naomba sana TFF tafuteni namna ya Kuwatuza, Nawahamasisha kila mtu mwenye mapenzi ba Nchi yeti, michezo ba vijana wetu pia watu wakichanga chochote walichonacho tunaweza kuwapatia vijana wetu motisha kubwa ,Mimi naanza ba Tshs.10,000.Vipngozi fungueni Account Wazalendo wenzangu wafuatao kuchanga na wadau wakubwa wajazie amigo mkubwa
Hongera sana sana vijana wetu mmetutoa kimasomaso.