RAIS Samia Suluhu Hassan amewapangia vituo vya kazi Mabalozi watatu na kumbadilishia kituo cha kazi Balozi mmoja. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Pia Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dk. Asha Rose Migiro amerejeshwa baada ya kumaliza mkataba wake huku Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Dk. Modestus Kipilimba akirejeshwa baada ya kustaafu.
Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus imefafanua mabalozi waliopangiwa vituo vya kazi kuwa ni; Balozi Khamis Mussa Omar kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China.
Omar anachukua nafasi ya Balozi Mbelwa Brighton Kairuki ambaye amehamishiwa London, Uingereza.
Balozi Ccaser Chacha Waitara kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Namibia. Bw. Waitara anachukua nafasi ya Balozi Dk. Modestus Kipilimba ambaye amestaafu.
Balozi Dk. Benard Yohana Kibesse kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Kenya. Balozi Kibesse anachukua nafasi ya Balozi Dk. John Stephen Simbachawene ambaye amehamishiwa Kampala, Uganda.
Balozi aliyehamishiwa kituo: Balozi Mbelwa Brighton Kairuki Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Uingereza. Balozi Kairuki anachukua nafasi ya Balozi Dk. Asha- Rose Migiro ambaye amemaliza mkataba wake.
Leave a comment