Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nape adai Dk. Slaa, wenzie wamekamatwa kwa tuhuma za uhaini, si kukosoa mkataba DP World
Habari za SiasaTangulizi

Nape adai Dk. Slaa, wenzie wamekamatwa kwa tuhuma za uhaini, si kukosoa mkataba DP World

Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Tekinolojia
Spread the love

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Dk. Willibrod Slaa, Boniface Mwabukusi na Mpaluka Nyangali ‘mdude’ wamekamatwa kwa tuhuma za uhaini na si sababu za kukosoa mkataba wa uwekezaji katika bandari ya Dar es Salaam kama inavyodaiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya kuibuka joto la kulaani kukamatwa kwa watatu hao pamoja na vinara wengine waliokuwa wanakosoa mkataba huo huku watetezi wa haki za binadamu wakiitaka serikali kuwaachia huru bila masharti yoyote.

Hata hivyo, katika taarifa  aliyoitoa leo Jumatano Nape amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumechanganya mambo mawili tofauti:

Mosi ni mjadala wa kitaifa unaoendelea kwa uwazi nchini Tanzania kuhusu mapendekezo

uwekezaji wa bandari kwa upande mmoja, na pili ni suala la kuvunjwa kwa sheria kwa upande mwingine.

Aidha, Nape amesema upotoshaji wa makusudi wa habari kuhusu hali halisi katika kukamatwa kwa washukiwa hao kunatia shaka nia na uaminifu ya mashirika mbalimbali nyuma ya taarifa hizo.

“Moja ya kauli za hivi majuzi kutoka kwa kundi la haki za kimataifa waliamua kupotosha ukweli kwa nia mbaya kwa kudai kwamba washukiwa walikamatwa kwa kukosoa tu mkataba wa bandari kati ya Tanzania na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).”

“Ukweli ni kwamba hakuna mtu yeyote ambaye amekamatwa nchini Tanzania wala hatokamatwa kwa kukosoa tu mpango wa uwekezaji bandarini au mradi wowote wa Serikali,” amesema Nape na kuongeza;

“Watu hao watatu waliohusika walikamatwa na Polisi kwa kutoa kauli za uchochezi hadharani… ambazo zinaweza kuleta vurugu na hata kuipindua Serikali ya wakati huo.”

Amesema washukiwa hao ambao baadhi yao walijaribu hadharani kuhamasisha raia kubeba silaha dhidi ya Jeshi la Polisi Tanzania, walikamatwa ili kutuma ujumbe mzito wa kuzuia uhalifu wowote ambao unahusishwa na makosa ya jinai.

Amesema kukamatwa huko hakuzuii kwa vyovyote vile uhuru wa kujieleza nchini Tanzania, lakini ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ili kuzuia machafuko ndani ya kijamii yanayoweza kutokea na kusababisha uasi dhidi ya serikali iliyochaguliwa kidemokrasia.

Kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulijiri baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camillius Wambura kudai kuwa wapo watu wanaotaka kuipindua Serikali kupitia ukosoaji wa uwekezaji kwenye bandari ya Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!