Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amepokea taarifa ya Maendeleo ya mazungumzo ya mchakato wa maridhiano ya kisiasa, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Desemba 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kwa mujibu wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu- Rais Samia amepokea taarifa hiyo kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana
Hii ni mara ya pili kwa Rais Samia kukutana na Mbowe kwa ajili ya mazungumzo hayo kwani mara ya kwanza, alikutana na Mbowe tarehe 4 Machi, 2022, Ikulu ya Dar es Salaam.
Mazungumzo hayo yalijiri saa chache baada ya Mbowe kuachiwa huru kutoka gerezani alikokaa kwa zaidi miezi tisa kwa tuhuma za ugaidi.
Pamoja na mambo mengine kikao chao hicho kilitajwa kufungua milango ya vikao vingine vya maridhiano ya kisiasa baina ya viongozi wa vyama hivyo.
Itakumbukwa kuwa Tume ya watu 10 kutoka Chadema iliundwa sambalba na idadi kama hiyo kutoka CCM na kukutana Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma kuanza mazungumzo hayo.
Licha ya Mbowe kupata upinzani kutoka kwa baadhi ya viongozi na wafuasi kutoka Chadema, mara kwa mara alisisitiza kuendelea na mazungumzo hayo kwani ndio njia sahihi ya kufikia muafaka.
Leave a comment