Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ampendekeza Dk. Mpango kuwa makamu wa Rais
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ampendekeza Dk. Mpango kuwa makamu wa Rais

Dk. Philip Mpango
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempendekeza Dk. Philip Mpango kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Jina hilo, limewasilishwa bungeni leo Jumanne tarehe 30 Machi 2021 na mpambe wa Rais kisha Spika wa Bunge, Job Ndugai akalitangaza mbele ya Bunge.

Mara baada ya jina hilo kutangazwa, Dk. Mpango ambaye ni waziri wa fedha na mipango, alishikwa na butwaa huku kelele za kushangilia zikitawala bungeni huku mteuliwa mwenyewe, akiwa amekaa akiwa haamini.

Dk. Mpango aliyezaliwa Jumapili tarehe 14 Julai 1957, ni mbunge wa Buhigwe mkoani Kigoma, anachukua nafasi ya Samia, aliyeapishwa kuwa Rais kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Saluhu akihutubia Taifa mara baada ya kuapishwa

Dk. Magufuli, alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwake Chato mkoani Geita.

Dk. Mpango aliingia bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2015, baada ya kuteuliwa na Rais Magufuli kisha akateuliwa kuwa waziri wa fedha na mipango, nafasi aliyoitumikia mpaka leo Jumanne.

Katika uchaguzi mkuu ulipita wa mwaka 2020, Dk. Mpango alirejea nyumbani kwao, Buhingwe kugombea ubunge na kushinda.

Kuteuliwa huko kuwa makamu wa Rais, kunalifanya jimbo la Buhingwe kuwa wazi hivyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kuitisha uchaguzi wa jimbo hilo.

Pia, nafasi ya waziri wa fedha na mipango nayo inakuwa wazi na Rais Samia atapaswa kuijaza.

Dk. Mpango, amewahi kuwa kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!