Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amng’ang’ania Jenerali Mabeyo
Habari za Siasa

Rais Samia amng’ang’ania Jenerali Mabeyo

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema bado ataendelea kumpa majukumu Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Venance Mabeyo kwakuwa bado ana nguvu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ameyasema hay oleo Alhamisi tarehe 30 Juni 2022 kwenye hafla ya kumwapisha Mkuu Mpya wa Majeshi Jenrali Jacob Mkunda na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Luteni Jenerali Salum Othman.

“Kama nilivyokuambia jana unaacha ukiwa kijana bado una nguvu na kwa maana hiyo tutaendelea kukuteua, tutaendelea kukupa majukumu uendelee kutusaidia, nadhani jioni ya leo Katibu Mkuu kiongozi utasikia kwenye bomba tayari ameshakupangia kazi ya kufanya,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema Jenerali Mabeyo amefanya kazi yake kwa uaminifu mkubwa “umetumikia cheo chako kwa jitihada kubwa na leo unamaliza na kukabidhi kwa wengine nakushukuru sana na nakupongeza sana kwasababu si kazi rahisi.”

Kwa upande wa CDF mpya Jenerali Mkunda na Mnadhimu Luteni Jenerali Othman, Rais Samia aliwapongeza na kuwatakiwa kazi njema na kwamba atazuungumza nao.

“Niwapongeze na niwatakie kazi njema mkaanze pale Jenerali Mabeyo alipoishia najua kwenye jeshi hakuna mtu kuingia na yake kama tulivyo kwenye Serikali-Rais Samia…maelekezo zaidi tutazungumza inbox kwa leo itoshe kuwapongeza na mfanye kazi kama aliyetoka na mkaendelee pale alipoishia,” amesema Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!