RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Profesa Maulid Mwatawala kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Elimu Tanzania (TET). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Uteuzi wa Profesa Mwatawala umeanza tarehe 30 Oktoba 2021, akichukua nafasi ya Profesa Bernadeth Kilian ambaye amemaliza muda wake.
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Jumanne, tarehe 2 Novemba 2021 na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu akiwa Glasgow nchini Scotland ambako Rais Samia yupo huko akihudhuria mkutano Mkutanowa 26 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP26).
Leave a comment