Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yajikita kileleni, yampiga Ruvu tatu
Michezo

Yanga yajikita kileleni, yampiga Ruvu tatu

Spread the love

 

 USHINDI wa mabao 3-1, dhidi ya Ruvu Shooting umzidi kuifanya klabu ya Yanga, kujichimbia kileleni kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiwa na pointi 15. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo ulipigwa hii leo, tarehe 2, novemba 2021kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Yanga ambao walikuwa wenyeji wa mchezo huo, walianza kwa kuruhusu bao mapema kipindi cha kwanza kupitia kwa Shabani Msala dakika ya 9’ na kisha Feisal Salum alifanikiwa kuisawazishia Yanga bao hilo dakika ya 33’ na kufanya mpira kwenda mapumziko wakiwa wamefungana bao 1-1.

Kipindi cha pili kilipo rejea, Shabani Djuma alifanikiwa kuindikia Yanga bao la pili kwa njia ya mkwaju wa penati kwenye dakika ya 48 ya mchezo.

Dakika 22’ baadae, Mukoko Tonombe ambaye leo aliingia kuchukua nafasi ya Khalid Aucho ambaye hakuwa sehemu ya mchezo huo kutokana na kupata majeraha aliandikia Yanga bao tatu na la mwisho kwenye mchezo huo.

Kwa matokeo hayo, Yanga sasa inafikisha jumla ya pointi 15, katika michezo mitano waliocheza, huku wakiwa wameruhusu bao moja tu, kuingia nyavuni mwao.

Mara baada ya mchezo huo Ligi Tanzania Bara itasimama kupisha michezo ya kimataifa na kurejea tena tarehe 20 Novemba, 2021 ambapo Yanga itashuka dimbani dhidi ya Namungo FC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!