Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amfuta kazi Mkurugenzi Mkuu TISS
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli amfuta kazi Mkurugenzi Mkuu TISS

Spread the love

RAIS wa Jamhuri, Dk. John Pombe Magufuli, amemfuta kazi aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Dk. Modestus Kipilimba. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais (Ikulu), jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi, tarehe 12 Septemba 2019, imeeleza kuwa nafasi ya Kipilimba imechukuliwa na Kamishena wa Polisi, Diwani Athuman Msuya.

Kabla ya uteuzi huo, Kamishena Diwani Msuya alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru).

Taarifa hiyo iliyotolewa na Gerson Msigwa, ambaye ni mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais, haikueleza sababu za rais kumfuta kazi Kipilimba.

Akizungumza baada ya kumuapisha kushika nafasi hiyo, Rais Magufuli, amemtaka Kamishena Diwani Athuman kuchapa kazi “kwa kuweka mbele maslahi ya taifa,”

Uteuzi wa Kamishena Diwani umeanza leo baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais amesema, Dk. Kipilimba atapangiwa kazi nyingine.

Kabla ya kufanywa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, tarehe 6 Septemba 2018, Kamishena Diwani Athumani alikuwa katibu tawala mkoa wa Kagera.

Alichukua nafasi ya ukurugenzi mkuu wa Takukuru, kutoka kamishena mwanzake wa Polisi, Valentino Mlowola, ambaye sasa amefanywa kuwa Balozi.

Kamishena Diwani Athuman amepata kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!