RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema anakwenda kufanya mabadiliko ya Wizara ya Afya kwa kuitenganisha na Maendeleo ya Jamii. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Rais Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 8 Machi 2022 wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kitaifa yamefanyika Unguja visiwani Zanzibar.
Rais Mwinyi alibainisha hayo kufuatia ombi la Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Dk. Doroth Gwajima la kutaka “pacha” mwenye jinsia yake.
“Nataka nimwambie kwamba hilo tayari limeshakaa vizuri. Mh. Mazrui (Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Nassor Ahmed Mazrui) amesema hakuwezi kwa sababu unazungumza sana, lakini na yeye kazungumza sana vilevile, kwa maneno tu mnawezana lakini leo nataka nimwambie yeye atabaki tu Wizara ya Afya lakini Maendeleo ya Jamii amwachie mtu mwingine,” alisema Dk. Mwinyi.
Leave a comment