Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Profesa Lipumba apata pigo la kufunga mwaka
Habari za Siasa

Profesa Lipumba apata pigo la kufunga mwaka

Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

CHAMA cha Wananchi (CUF), upande unaongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba kimepata pigo kubwa baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kupiga marufuku bodi yake kujihusisha na shughuli zozote za chama hicho mpaka shauri la msingi litakapomalizika, anaandika Hamisi Mguta.

Profesa Lipumba ambaye anatambuliwa na msajili wa vyama siasa nchini analumbana na Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Shariff Hammad hatua ambayo imesababisha pande hizo mbili kufikishana mahakamani ili kutafuta haki.

Awali, mahakama hiyo iliyatupilia mbali maombi ya Wakili Mashaka Ngole (anayemwakilisha Lipumba) aliyokuwa anaomba Jaji asisome maamuzi hayo kwa madai kuwa Lipumba anakusudia kukata rufaa juu ya maamuzi ya Jaji kukataa kujitoa kusikiliza mashauri ya CUF.

Mahakama Kuu imesema, hakuna hoja za kisheria zinazoizuia kuacha kuendelea na shughuli ilizozipanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!