Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Muhongo awakalia kooni REA
Habari Mchanganyiko

Prof. Muhongo awakalia kooni REA

Fundi umeme wa Tanesco akiunganisha umeme wa REA katika moja ya nyumba zilizopo kijijini
Spread the love

WAZIRI wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ameiagiza bodi mpya ya wakurugenzi wa Wakala wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA) kuwakagua wakandarasi wote ambao wamepata tenda ya usambazaji wa umeme vijijini, anaandika Dany Tibason.

Mbali na kutoa agizo la kuwakagua wakandarasi pia REA wametakiwa kuhakikisha wanatumia vifaa vinavyozalishwa ndani ambavyo vina ubora badala ya kuagiza vifaa vya umeme kutoka nje ya nchi.

Akizungumza na wajumbe wapya wa Bodi mpya REA, Prof. Muhongo amesema bodi hiyo inatakiwa kuwa na malengo mapana kwa ajili ya kuhakikisha umeme unawafikia wananchi kwa kiwango kikubwa.

Prof. Muhongo amewataka wajumbe hao wa bodi kuhakikisha wanapokea makablasha kabla ya wiki mbili ili waweze kuyapitia mapema na kuyasoma.

Katika kuhakikisha umeme unakuwa kichocheo cha maendeleo ni vyema umeme huo ukawekewa katika taasisi mbalimbali ili kuwapatia umeme.

“Sasa katika kutekeleza umeme unakuwa kichocheo, ni vyema umeme usivuke taasisi mbalimbali kama vile, shule zote za sekondari na shule za msingi, zahanati hospitali, mashamba makubwa na katika sehemu za kibiashara,” amesema.

Katika uzinduzi huo Prof. Muhongo, ameitaka bodi hiyo kuhakikisha inasimamia zaidi ubora wa vifaa vya umeme ambavyo vina ubora.

“Nawaagiza nyie bodi kuhakikisha mnaponunua vifaa vya umeme kuhakikisha vinakuwa na ubora na vinavyozalishwa,” amesema Prof. Muhongo.

Aidha amesema makampuni yote ya kutoka nje ya nchi ambayo yanafanya kazi ndani ni lazima kuwa na wakandarasi wadogo wa ndani na si vinginevyo.

“Haiwezekani kwa mfano nguzo za umeme zinapatikana hapa Iringa, lakini unaweza kushanga eti nguzo zinaagizwa kutoka Afrika Kusini na maeneo mengine,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!