Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Pombe za viroba, bangi zazua balaa Morogoro
Habari Mchanganyiko

Pombe za viroba, bangi zazua balaa Morogoro

Pombe zilizofungashwa katika mifuko ya nailoni maarufu kama Kiroba
Spread the love

OPERESHENI ya kukamata pombe ambazo hufungwa katika vifuko maalum maarufu kama viroba, imeendelea kushika kasi mkoani Morogoro ambapo sasa jeshi la polisi limewakamata jumla ya wafanyabiashara 14 waliokutwa na pombe hizo, anaandika Christina Haule.

Watu hao 14 wanatuhumiwa kukutwa na pombe kali za Viroba katoni 128, dazeni 11, pakiti 16 na vifungashio 7 katika maeneo mbalimbali mkoani Morogoro.

Urlich Matei, Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro amesema polisi walianza operesheni dhidi ya pombe kali za vifungashio vya plastiki maarufu kwa jina la Viroba tarehe 3 Machi mwaka huu.

“Tumefanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao katika maeneo mbalimbali ya mkoa, wakiwa na viroba vya aina mbalimbali zikiwemo Value, Zed, Nguvu Spirit, Kiroba Original, Konyagi na Vodka.

“Watuhumiwa tuliowakamata wanaendelea kuhojiwa na polisi huku hatua za kuwafikisha mahakamani zikiendelea,” amesema.

Kamanda Matei pia ametangaza kuwa jeshi hilo linawashikilia watu wengine 16 kwa kukamatwa na bangi katika kijiji cha Singisa wilayani Morogoro vijijini.

“Tukio hilo lilitokea tarehe 08 Machi 8, watuhumiwa 11 walikamatwa wakiwa na viroba 31 vya kilogramu 50 za bangi iliyochambuliwa kwa ajili ya matumizi, misokoto 641 na miche ya bangi 26.
“Polisi waliokuwa doria katika maeneo hayo walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine watano wakiwa na bangi kwenye viroba 31 vyenye ujazo wa kilogramu 50 kila kimoja,” amesema Kamanda Matei.

Imeelezwa kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakijiandaa kusafirisha mizigo hiyo kwa kutumia pikipiki yenye namba za usajili MC880 BLT na T478 BWH aina ya Sanya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!