JESHI la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, linawashikilia watu 12 Wilaya ya Hai kwa mahojiano wakituhumiwa kufanya vurugu na kushambulia kwa mawe mkutano wa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu alipokuwa akitafuta wadhamini. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Vurugu hizo zilitokea tarehe 14 Agosti 202 wilayani Hai ambapo zilisababisha majeruhi wanne waliojeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao na kulazwa hospitali ya Wilaya hiyo.
Katika vurugu hizo, baadhi ya magari yariharibika kutokana na kupondwa kwa mawe.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili 23 Agosti 2020, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Emmanuel Lukula amesema, jana Jumamosi ulifanyika msako mkali na kuwakamata watuhumiwa hao ambao kwa sasa wanahojiwa na watafikishwa mahakamani.
”Nitoe wito kwa wananchi na wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu hasa tunapoelekea kwenye kampeni za uchaguzi mkuu zitakazoanza 26 Agosti 26, 2020,” amesema Lukula
”Jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro tumejipanga kuhakikisha amani zinatawala wakati wote kwa atakayeenda kinyume na sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi tutakabiliana naye kwa nguvu zote na bila huruma kwa mujibu wa sheria,” amesema Lukula.
Leave a comment