Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi yawadaka 12, tuhuma kuvuruga mkutano wa Lissu
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Polisi yawadaka 12, tuhuma kuvuruga mkutano wa Lissu

Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, linawashikilia watu 12 Wilaya ya Hai kwa mahojiano wakituhumiwa kufanya vurugu na kushambulia kwa mawe mkutano wa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu alipokuwa akitafuta wadhamini. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Vurugu hizo zilitokea tarehe 14 Agosti 202  wilayani Hai ambapo zilisababisha majeruhi wanne waliojeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao na kulazwa hospitali ya Wilaya hiyo.

Katika vurugu hizo, baadhi ya magari yariharibika kutokana na kupondwa kwa mawe.

Akizungumza na waandishi wa habari  leo Jumapili 23 Agosti 2020, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Emmanuel Lukula amesema, jana Jumamosi ulifanyika msako mkali na kuwakamata watuhumiwa hao ambao kwa sasa wanahojiwa na watafikishwa mahakamani.

”Nitoe wito kwa wananchi na wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu hasa tunapoelekea kwenye kampeni za uchaguzi mkuu zitakazoanza 26 Agosti 26, 2020,” amesema Lukula

”Jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro tumejipanga kuhakikisha amani zinatawala wakati wote kwa atakayeenda kinyume na sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi tutakabiliana naye kwa nguvu zote na bila huruma kwa mujibu wa sheria,” amesema Lukula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

error: Content is protected !!