Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wavamia mkutano wa Zitto
Habari za Siasa

Polisi wavamia mkutano wa Zitto

Spread the love

MAOFISA kutoka Jeshi la Polisi limevamia Makao Makuu ya Chama cha ACT-Wazalendo na kuondoka na Ado Shaibu, Katibu wa Itikadi na Uenezi. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Tukio hilo limetokea asubuhi ya leo tarehe 16 Agosti 2019, siku ambayo Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa chama hicho alipanga kufanya mkutano na wanahabari kwa ajili ya kuzungumzia Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Kabla ya mkutano huo kuanza, polisi waliovaa mavazi ya kiraia wakiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni RCO, John Malulu waliwatawanya waandishi wa habari waliokuwa wanasubiri mkutano huo uliotarajia kuanza saa tano asubuhi.

RCO Malulu aliwatawanya wanahabari pasipo kuwaeleza sababu za kuchukua uamuzi huo.

“Naomba waandishi mtawanyike hili jambo linalotakiwa kufanyika lisimame, nadhani nimeeleweka,” RCO Malulu aliwaambia waandishi.

Kabla ya kukamatwa, Ado aliwaeleza wanahabari kwamba polisi waliwataarifu kwamba, wanahitaji kiongozi yeyote wa chama chao kufika katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay kwa ajili ya mahojiano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!