MAOFISA kutoka Jeshi la Polisi limevamia Makao Makuu ya Chama cha ACT-Wazalendo na kuondoka na Ado Shaibu, Katibu wa Itikadi na Uenezi. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).
Tukio hilo limetokea asubuhi ya leo tarehe 16 Agosti 2019, siku ambayo Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa chama hicho alipanga kufanya mkutano na wanahabari kwa ajili ya kuzungumzia Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Kabla ya mkutano huo kuanza, polisi waliovaa mavazi ya kiraia wakiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni RCO, John Malulu waliwatawanya waandishi wa habari waliokuwa wanasubiri mkutano huo uliotarajia kuanza saa tano asubuhi.
RCO Malulu aliwatawanya wanahabari pasipo kuwaeleza sababu za kuchukua uamuzi huo.
“Naomba waandishi mtawanyike hili jambo linalotakiwa kufanyika lisimame, nadhani nimeeleweka,” RCO Malulu aliwaambia waandishi.
Kabla ya kukamatwa, Ado aliwaeleza wanahabari kwamba polisi waliwataarifu kwamba, wanahitaji kiongozi yeyote wa chama chao kufika katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay kwa ajili ya mahojiano.
Leave a comment