Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi waendelea kuwabana wanavunja sheria, operesheni 3D yaendelea
Habari Mchanganyiko

Polisi waendelea kuwabana wanavunja sheria, operesheni 3D yaendelea

Spread the love

 

JESHI la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Kimeendelea na operesheni ya kutoa elimu na kuwakamata wale wote wanaoendelea kuvunja sheria za usalama Barabarani huku Jeshi hilo likiwapongeza wale wote waliotii agizo la serikali la kuondoa namba ambazo hazijasibitishwa na mamlaka ya viwango Tanzania (TBS). Anaripoti bel Paul, Jeshi la Polisi Arusha … (endelea).

Akiwa katika Operesheni hiyo leo tarehe 19 Machi, 2024 Mkoani Arusha, Mkuu wa Operesheni za kikosi cha Usalama barabarani nchini kamishna msaidizi wa Polisi ACP, Nasoro Sisiwayah amesema kikosi hicho kinaendelea kuwakamata wale wote walio kaidi agizo la kuondoa namba zenye ujazo 3D na ving’ora.

ACP Sisiwayah ameongeza kuwa operesheni hiyo imelenga pia kukamata madeni ya wale wote waliofanya makosa barabarani na kupigwa faini ambapo amebainisha kuwa zoezi hilo linaendela nchi nzima huku akiwaomba watumiaji wa vyombo vya moto ambao wanadaiwa kuhakikisha wanalipa madeni yao kwa wakati.

Aidha amesema kuwa operesheni hiyo pia imehusisha kuwakamata wale wote wanaoendesha mwendo kasi vyombo vya moto ambapo amebainisha kuwa uchunguzi wa Jeshi hilo unapofanyika umebaini kuwa chanzo cha ajali nyingi ni mwendo kasi hivyo nao watakamatwa.

Nao baadhi ya madereva licha ya kupongeza operesheni hiyo wamebainisha kuwa undoshaji wa namba hizo utasaidia katika swala la ulinzi na usalama huku wakiliomba Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani kuendelea na operesheni hiyo ambayo itasaidia katika usalama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

error: Content is protected !!