Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jela miaka 25 kwa kukutwa na kilo 107.29 za bangi
Habari Mchanganyiko

Jela miaka 25 kwa kukutwa na kilo 107.29 za bangi

Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, kanda ya Morogoro imemhukumu miaka 25 jela John Mwaseba Mwasikili baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya aina ya bangi zenye ujazo wa kilo 107.29. Anaripoti Yusuph Kayanda, Morogoro … (endelea).

Akitoa hukumu hiyo Jaji wa mahakama hiyo, M. P.Otaru amesema ushahidi uliotolewa na mashahidi 16 na vielelezo 15 vya upande wa mashitaka haukuacha shaka dhidi ya mshitakiwa kutenda kosa hilo.

Jaji Otaru amesema kuwa amemtia hatiani mshtakiwa huyo baada ya kujiridhisha kuwa ni kweli mshitakiwa alikamatwa na dawa ya kulevya aina ya bangi yenye uzito wa kilogram 107.29 iliyokuwa ndani ya gari aina ya Toyota Kluger namba T.895 CQR kwenye mifuko nane ya sulphate.

Mahakama pia imeamuru gari namba T 895 CQR ambalo lilikuwa na bangi hiyo litaifishwe na kielelezo ambacho ni dawa za kulevya aina ya bangi kuteketezwa.

Mshitakiwa Mwasikili alikamatwa na Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya na kufikisha katika Mahakama kuu kanda ya Morogoro Machi 15, 2024.

Inadaiwa kuwa mwaka 2022 huko Morogoro lilikamatwa gari aina ya Toyota Kluger lenye namba za usajili T.985 ambalo ndani yake lilikutwa na mifuko nane ya sulphate ikiwa na dawa za kulevya aina ya bangi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!