Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mahakama yamhukumu mwandishi wa habari kifungo cha miezi 6
Habari Mchanganyiko

Mahakama yamhukumu mwandishi wa habari kifungo cha miezi 6

Spread the love

Mahakama ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imemhukumu kifungo cha miezi sita jela mwandishi wa habari wa Congo, Stanis Bujakera baada ya kukutwa na hatia ya kueneza habari za uongo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Bujakera, Jean-Marie Kabengela amesema jana Jumatatu majaji wametoa adhabu hiyo ya kifungo cha miezi sita pamoja na  kulipa faini ya faranga milioni 1 za Congo sawa na Sh 940,000.

Aliongeza kuwa Bujakera, ambaye anafanya kazi katika vyombo vya habari vya kimataifa ikiwa ni pamoja na Jeune Afrique na Reuters, anatarajiwa kuondoka katika gereza ambalo amekuwa akishikiliwa tangu Septemba mwaka jana kwa sababu tayari ameshatumikia muda huo.

Wakili huyo alisema, kwa kuzingatia taratibu za kawaida katika kesi hizo, timu ya mawakili inayomwakilisha Bujakera itarejea tena mahakamani hapo leo Jumanne, kupata nakala ya uamuzi huo na kulipa faini hiyo ili aachiliwe.

Bujakera, ambaye amekana mashtaka yote, alikamatwa katika mji mkuu Kinshasa kwa tuhuma za kueneza habari za uongo kuhusu mauaji ya mwanasiasa mashuhuri wa upinzani katika makala iliyochapishwa na Jeune Afrique, gazeti la habari la Ufaransa limesema.

Mwendesha mashtaka katika kesi hiyo mapema mwezi huu alikuwa ameitaka mahakama ya Kinshasa kumhukumu Bujakera kifungo cha miaka 20 jela.

Mashirika ya haki za ndani na kimataifa yakiwemo Reporters Without Borders na Amnesty International yalilaani kuzuiliwa kwa Bujakera, na kuliita shambulio dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!