Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pigo CCM, Mzee Seif Khatibu afariki
Habari za SiasaTangulizi

Pigo CCM, Mzee Seif Khatibu afariki

Dk. Khatibu (kulia) alipomkabidhi fomu ya kuwania urais, Dk. John Pombe Magufuli mwaka 2015
Spread the love

 

DAKTARI Mohmmed Seif Katibu, aliyewahi kuwa Mkuu wa Oganizesheni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na waziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nyakati tofauti, amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Tayari taarifa za kifo hicho zilizotolewa na familia yake leo Jumatatu tarehe 15 Februari 2021, zimeeleza Mzee Seif alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Al Rahma, Kilimani visiwani Zanzibar mpaka mauti yanamkuta, mapema leo asubuhi.

Mzee Seif Khatibu mapaka anafikwa na mauti, alikuwa Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) na mmiliki na Mkurugenzi wa Zanzibar Media Group inayomiliki Kituo cha Redio cha Zenj FM, TV na Gazeti la Nipe Habari,

Katika maisha yake ya siasa, Mzee Seif Khatibu alikuwa Mtu wa karibu na mtiifu kwa Mwalimu Julius Nyerere, Rais wa kwanza wa Tanzania, alikuwa mjumbe katika Juuiya ya Umoja wa Vijana Tanzania (UVT) kabla ya kubadilisha na kuwa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Dk. Muhammed Seif Khatib alipotunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Mkuu wa Chuo hicho, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, 25 Novemba 2011.

Mzee Khatibu aliwaki kuongoza wizara mbalimbali Bara na Visiwani ambapo pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Uzini, Zanzibar

Pia, aliuwa mshairi na Mhadhir katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Aliwahi kuwa mwanasoka aliyechezea Klabu ya Kikwajuni Sport na Timu ya Taifa ya Zanzibar. Mzee Seif Khatibu pia aliwahi kuimba taarabu.

Mwaka 2015, wakati wa mchakato wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu za wagombea urais ndani ya CCM, Dk. Khatibu akiwa, Mkuu wa Oganizesheni wa chama hicho, alikuwa na jukumu la kuwapatia fomu wagombea wote waliojitokeza zaidi ya 38 akiwemo, Dk. John Pombe Magufuli, ambaye baadaye aliibuka mshindi wa Urais.

Dk. Khatibu amewahi kuwa Mjumbe wa Halmashuari Kuu ya CCm, kati ya mwaka 1978 hadi 2017, Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hichokati ya mwaka 1995 hadi 2017) na baadaye akwa katibu wa Oganaizesheni kati ya 2012 na 2017.

Khatibu, alikuwa mtunukiwa wa kwanza wa shahada ya uvamivu (PhD), katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), tarehe 25 Novemba 2011 na alitunukiwa shahada hiyo na aliyekuwa mkuu wa chuo hicho, Hayati Benjamin Willim Mkapa.

1 Comment

  • Changamoto ya kupumua? Au Covid 19? Siku zote mnatuambia eti msema kweli ni mpenzi wa …….

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!