Winga wa kimataifa wa Malawi Peter Banda, amekuwa mchezaji wa kwanza kufungua dirisha la usajilin ndani ya klabu ya Simba mara baada ya kutambulisha hii leo kama mchezaji mpya ndani ya kikosi hiko. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)
Usajili wa kinda hilo (20), umekuwa wa kwanza ndani ya klabu hiyo toka kufunguliwa kwa dirisha la usajili tarehe 19 Julai 2021.
Mchezaji huyo ambaye anamilikiwa na klabu ya Nyasa Bullets ya nchini Malawi, amejiunga na Simba akitokea kwenye klabu ya Sherrif FC ambapo alipokuwa akicheza kwa mkopo na mkataba wake kumalizika.
Kusajiliwa kwa winga huyo, huwenda kukawa mwisho wa nyota kutoka nchini Zimbabwe Perfect Chikwende ambaye alisajiliwa kwenye dirisha dogo na kushindwa kuonesha makali yake.
Mchezaji huyo amejiunga na mabingwa hao wa Ligi Kuu kewa mkataba wa miaka mitatu.
Leave a comment