Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Biashara NMB yakabidhi mabati 200, kompyuta 25 shule za Babati
Biashara

NMB yakabidhi mabati 200, kompyuta 25 shule za Babati

Meneja wa Benki ya NMB kanda ya Kaskazini, Dismas Prosper (aliyesimama) akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mabati 200 na Kompyuta 25 kwa shule za Wilaya ya Babati. Watatu kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Babati, Lazaro Twange na wapili kulia ni mkurugenzi wa Wilaya ya Babati, Anna Fisso
Spread the love

BENKI ya NMB Kanda ya Kaskazini nchini Tanzania imekabidhi msaada wa bati 200 kwa Shule ya Sekondari Olongadida, kata ya Qash na kompyuta 25 kwa shule saba zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara ili kusaidia kuboresha utoaji wa elimu kwa wanafunzi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Msaada huo imekabidhiwa na Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Dismas Prosper kwa mkuu wa wilaya ya Babati, Lazaro Twange.

Meneja wa Benki ya NMB kanda ya Kaskazini, Dismas Prosper(watatu kutoka kulia) akikabidhi kompyuta kwa wa walimu wa sekondari na shule za msingi,watatu kutoka kulia ni Mbunge wa jimbo la Babati Mjini Paulina Gekul .Benki ya Nmb imekabidhi jumla ya kompyuta 25 na mabati 200 kwa shule mbalimbali wilayani Babati.

Prosper alisema lengo la kutoa msaada huo ni baada ya kuona vikwazo vinavyowakabili wanafunzi katika wilaya ya Babati ambao walikuwa wanatembea umbali mrefu kwenda shule lakini kwa ukosefu wa kompyuta zinazosaidia katika utoaji wa elimu ya kidigitali.

Alisema, “wanafunzi wa maeneo haya wanasafiri umbali mrefu sana kwenda shule sababu ujenzi wa shule ya karibu haujakamilika, hivyo tumeleta mabati haya ili kukamilisha ujenzi wa shule hizi na kuwapunguzia wanafunzi wetu umbali wa kutembea kwenda shuleni.”

“Dunia ya sasa ni ya kiteknolojia zaidi na ndio maana tukaona tukubaliane na maombi ya shule za wilaya ya Babati kupata kompyuta ili kurahisisha ufundishaji wa somo hilo na kupunguza uhaba wa vifaa hivi katika shule zetu,” Alisema

Aidha Meneja huyo alisema lengo la kutoa msaada huo ni kwa ajili ya kusaidiana na serikali katika kutatua changamoto za wananchi hasa katika sekta ya elimu na afya huku akisema NMB kwa mwaka huu wametenga Sh.2 bilioni ili kuboresha huduma hizo kwa nchi nzima.

Naye mkuu wa wilaya ya Babati Lazaro Twange akipokea msaada huo katika Kijiji cha Olongadida, aliipongeza NMB kwa kuwa mshirika mwema wa maendeleo ya wilaya ya Babati.

Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini Paulina Gekul akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya Kompyuta 25 zilizoyolewa na Benki ya NMB kwa shule za msingi na sekondari za wilaya ya Babati,Watatu kutoka kulia ni Meneja wa Benki ya NMB kanda ya kaskazini Dismas Prosper.

Alisema serikali itaendelea kuzungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa ajili ya kuendelea kutoa misaada kwa shule za wilaya hiyo.

Aidha, Twange aliwapongeza wananchi wa Kijiji hicho kwa kuchanga  Sh.20 milioni pamoja na kutumia nguvu zao binafsi kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Olongadida.

Mkazi wa Kijiji cha Olongadida Hamis Rajab aliishukru NMB kwa kutoa msaada huo na kudai utasaidia kukamilisha haraka ujenzi wa shule hiyo na ili kusaidia wanafunzi waache kutembea umbali wa kilometa nane.

Akizungumza baada ya kupokea misaada hiyo, Mbunge wa Babati ambaye pia ni naibu waziri wa utamaduni, sanaa na michezo, Pauline Gekul aliwataka walimu wakuu kuzitunza vizuri kompyuta hizo ili zikasaidie idadi kubwa ya wanafunzi wanaopita katika shule hizo.

Kwa upande wake, kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Anna Fissoo aliwapongeza NMB kwa msaada huo na kuahidi kutunza vifaa hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Jiandalie Strawberry Cocktail yako nyumbani huku unacheza kasino 

Spread the love  UTAANDAA matunda yako unayotaka kutumia unaweza kutumia Strawberry, Cantaloupe...

Biashara

420 Blaze It chimbo jipya la kuchota mihela Meridianbet kasino 

Spread the love  JE, umewahi kucheza mchezo wa droo wenye droo 10?...

Biashara

Exim yawainua kiuchumi wanawake wajasiriamali kupitia mpango wa WEP

Spread the love  BENKI ya Exim kupitia Mpango wake wa Kuwawezesha Kiuchumi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!