Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Viongozi CCM watakiwa kukubali kupingwa uchaguzi
Habari za Siasa

Viongozi CCM watakiwa kukubali kupingwa uchaguzi

Spread the love

VIONGOZI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) waliopo madarakani wametakiwa kuruhusu watia nia wa nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho kuchukua fomu hata katika  nafasi watakazozitetea na kwamba kufanya hivyo watakuwa wametenda haki. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Hayo yalielezwa na diwani wa Kata ya Chanika Wilaya ya Ilala, mkoa wa Dar es salaam, Masaburi Ojambi,  wakati akifungua semina kwa makada wa CCM ngazi ya matawi na Kata iliyofanyika  leo Jumanne tarehe 9 Mei 2022 kwenye Kata hiyo.

Ojambi alieleza kuwa makatibu waache kasumba ya kuficha fomu kwa nafasi ambazo wanatarajia kuzitetea katika chaguzi unaoendelea hivisasa ndani ya chama hicho na badala yake watoe fursa kwa kila mhitaji ili demokrasi ichukuwe sehemu yake.

Mtoa mada katika semina hiyo, Mwinyimkuu Sangala aliwataka viongozi kufuata maadili na kanuni za chama kwa kupitisha wagombea wenye sifa na hivyo watakuwa wametenda haki na kupunguza malalamiko kwa watu wengine.

Hata hivyo aliwataka vijana kukimbilia kwenye vyuo vya ufundi stadi watakakoenda kupata ujuzi wa fani mbalimbali kwa ajili ya kuendesha maisha yao ya kila siku  huku wakiongeza pato la taifa kwa kuwa watakuwa wanalipa kodi na ushuru kutokana na kazi watakazozifanya.

Naye mwenyekiti wa taasisi ya Elimu ya Furahika, Mohamed Ngwenje alitumia nafasi hiyo kutangaza ofa kwa vijana 250 ambao alidai watasoma bure kwenye chuo cha ufundi kinachoendeshwa na taasisi hiyo lengo ni kuwaandaa katika maisha ya kujitegemea.

Ngwenje  alieleza fursa  hiyo kwamba inatolewa kwa kila mwaka na kwamba kinachotakiwa kwa wazazi ni  kuwanunulia watoto wao vifaa vya kazi watakayojifunza kwa kipindi hicho huku gharama za chuo zikilipwa na taasisi hiyo ya Elimu ya Furahika.

Aidha katibu wa mbunge wa jimbo la Ukonga, Jemes  Uliuma alitoa pole kwa wakazi wa Kata ya Chanika na  Zingi waliopatwa na janga la panya road huku akieleza azma ya mbunge kuzitembelea kwa ajili ya kujua changamoto walizonazo.

Uliuma alisema wananchi wa Kata hizo walivamiwa na vijana wa panya road na kushambuliwa kwa mapanga na marungu kitendo ambacho licha ya mbunge huyo kulaani lakini pia kimemfanya kuandaa ziara ya kwenda kwenye maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!