BENKI ya NMB kupitia matawi yake yote nchini inatarajiwa kuanza rasmi Jumatatu tarahe 10 Julai 2023, kusajili na kutoa kadi za uanachama wa Klabu ya Yanga. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 8 Julai 2023 na Idara ya Mawasiliano ya benki hiyo, mwanachama wa Yanga akifungua akaunti atalipia Sh. 34,000 kama kianzio cha kupata kadi ya Yanga (Sh. 5,000 ni malipo ya kadi, Sh. 5,000 amana ya kuanzia na Sh. 24,000 ni ada ya mwanachama kwa mwaka mzima).
Taarifa hiyo imeeleza kuwa mwanachama wa Yanga atalipia Sh. 29,000 kama kianzio cha kupata kadi ya Yanga ambayo ni kadi ya malipo ya kabla (Prepaid Card) Sh. 5,000 ni malipo ya kadi na Sh. 24,000 ni ada ya mwanachama kwa mwaka mzima).
“Kadi hizi hazitakua za uanachama/ushabiki tu, pia zina uwezo wa kufanya kazi kama kadi ya Benki! Unaweza kufanya miamala yote ya kibenki ikiwemo kuiwekea pesa, kutoa hela katika ATM na kufanya malipo mtandaoni na katika vituo vya malipo (POS).
“Wanachama wanaweza kupata kadi za malipo ya kabla ambayo huitaji kuwa na akaunti nasi na kufanya malipo kwa kupitia mtandao au kwenye Point of Sales (POS),” imeeleza taarifa.
Aidha, imefafanuwa kuwa wanachama wa Yanga watanufaika na huduma na ofa mbalimbali za NMB ikiwemo mikopo isiyokua na dhamana (Mshiko Fasta) na punguzo la bei wakifanya malipo kupitia NMB Lipa Mkononi (QR).
Mbali na huduma za uanachama, NMB itaanzisha bima ya mwananchi ambayo itakua na gharama nafuu.
Leave a comment