MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Charles Kicheere amesema ukaguzi wa mfumo wa ulipaji wa Mfuko wa Bima ya Afya kwa watoa huduma ulibaini madai yasiyostahili kwa vituo vya huduma ya afya toka mwaka 2019 hadi 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Alibainisha hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akiwasilisha Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa mwaka 2021/22 kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
Alisema mfuko ulilipa madai yasiyostahili tangu ta Sh 10.3 bilioni kwa vituo binafsi, Sh 1.58 kwa vituo vya Serikali na Sh 2.49 kwa vituo vya taasisi za kidini.
“NHIF ililipa madai kwa vituo vya afya visivyostahili baada ya kugundua tatizo hilo ni vituo vichache vilirejesha baadhi ya fedha na Sh 7 bilioni hazikurejeshwa na hakuna hatua iliyochukuliwa kwa watumishi walihusika,” alisema Kicheere.
Katika hatua nyingine CAG Kichere alisema ukaguzi umebaini kuwa matumizi kutoa huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya yamekuwa makubwa ikilinganishwa na michango yao.
Katika mwaka 2021/2022 mfuko umepata hasara ya Sh189.65 bilioni ikilinganishwa na Sh93.6 bilioni iliyokuwapo mwaka uliotangulia.
“Pia mfuko umekuwa na mtiririko hasi wa fedha katika shughuli zake za uendeshaji, mwenendo huu unaonyesha kuwa michango inaongezeka kwa asilimia 12.9 wakati matumizi yanaongezeka kwa asilimia 24.6 mara mbili,” alisema Kichere.
Alisema makadirio ya uwezo wa mfuko kujiendesha kwa Juni 30, 2021 unaonyesha kuwa mapato ya mfuko yataendelea kuwa chini ya matumizi kwa siku zijazo na mfuko utatumia ziada iliyokusanywa jambo ambalo litasababisha ukwasi kuwa hasi ifikapo mwaka 2025.
“Napendekeza kufanyiwa kazi kwa mapendekezo ya ripoti ya wataalamu na kutekeleza yaliyohitajika ili kurekebisha nakisi kama vile kuimarisha usimamizi wa utoaji huduma za afya,” alisema.
Hello:- Pata dollar za Marekani milion 10 kutoka kwenye Bank yetu……. UTAPATAJE FEDHA HIZI
https://www.news24.com/citypress/news/gauteng-health-concerned-by-unclaimed-corpses-gathering-in-mortuaries-20220323