Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC CCM yateua wagombea uenyekiti mikoa, wilaya
Habari za Siasa

NEC CCM yateua wagombea uenyekiti mikoa, wilaya

Spread the love

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefanya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa leo Jumatano kufanya uteuzi wa mwisho wa wagombea wa nafasi za uongozi ndani ya chama kwa ngazi ya mkoa na wilaya.

Nafasi zinalenga kujaza nafasi zilizoachwa wazi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo na uteuzi wa nafasi nyingine. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Paul Makonda amesema nafasi ya mwenyekiti wa mkoa wa Arusha: wanachama waliojitokeza 89.

Walioteuliwa ni: Dk. Daniel Mirisho Pallangyo, Loy Thomas Sabaya, Solomon Olesendeka Kivuyo na Edna Israel Kivuyo.

Mkoa wa Mbeya: Wanachama waliojitokeza 48, Walioteuliwa ni:  Felix Jackson lyaniva,  Patrick Adkin Mwalunenge na Fatuma Ismail Kasenga.

Mkoa wa Mwanza: Wanachama waliojitokeza 109, Walioteuliwa ni: Michael Lushinge Masanja (Smart),  Sabana Lushu Salinja, Dkt. Anjelina William Samike, Elizabeth Watson Nyingi na David Mayala Mulongo.

Nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya

Wilaya ya Mpanda: Wanachama waliojitokeza 36, Walioteuliwa ni:  Hamis Chande Soud, Joseph Aniseth Lwamba, Josephina Yusuph Baraga na Emmanueli David Manamba.

Wilaya ya Kusini Unguja: Wanachama waliojitokeza 15, Walioteuliwa ni: Maryam Suleiman Haji, Ali Timamu Haji na Mohammed Haji Hassan.

Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kimepongeza Serikali inayoongozwa na Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!