Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Ndayiragije aibukia Geita Gold
Michezo

Ndayiragije aibukia Geita Gold

Etienne Ndayiragije, Kocha wa Taifa Stars
Spread the love

 

KLABU ya Geita Gold imemtangza rasmi aliyekuwa kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Etienne Ndayilagije kuwa kocha mkuu wa kikosi hiko mara baada ya kusaini mkataba. Anaripoti Mwandishi Wetu….(endelea)

Klabu hiyo itacheza Ligi Kuu soka Tanzania Bara kwa mara ya kwanza kwenye msimu ujao, toka ilipopanda daraja kwenye Ligi Kuu, ikitoka Ligi daraja la kwanza kwenye msimu wa 2020/21.

Geita Gold iolimtangaza kocha huyo, kupitia kurasa zao za kwenye mitandao ya kijamii, bila kueleza ni mkataba wa muda gani.

Ndayiragije ambaye ni raia wa Burundi anarejea tena nchini Tanzania mara baada ya kutimuliwa kama kocha mkuu kwenye kikosi cha Taifa Stars Februari, mwaka huu kufuatia kupata matokeo mabovu kwenye michuano ya kombe la mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) iliyofanyika nchini Cameroon, mwaka jana.

Hii itakuwa klabu yake ya nne kufundisha ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara, kufuatia kuzinoa klabu kama Mbao Fc, Kmc na Azam FC

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!