Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR- Mageuzi yafanya mabadiliko ya uongozi
Habari za SiasaTangulizi

NCCR- Mageuzi yafanya mabadiliko ya uongozi

James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi
Spread the love

CHAMA cha NCCR- Magezi, nchini Tanzania, kimefanya mabadiliko makubwa katika uongozi wake wa kitaifa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika mabadiliko hayo, Martha Chiomba, ambaye alikuwa mgombea ubunge katika jimbo la Kawe, kwenye uchaguzi mkuu uliyopita, amepitishwa kuwa katibu mkuu mpya wa chama hicho.

Chiomba ambaye alitikisa kampeni za uchaguzi katika jimbo la Kawe, kutokana na staili yake ya kampeni za “nyumba kwa nyumba,” amechukua nafasi hiyo, kutoka kwa Elizabeth Mhagama.

Taarifa zinasema, Elizabeth amefikia maamuzi ya kujiuzulu wadhifa huo, kutokana na kutingwa na majukumu yake binafsi na yale ya familia.

Martha Chiomba

Elizabeth Martin Mhagama, ni wakili wa kujitegemea, anayeyefanyia shughuli zake jijini Dar es Salaam, ambaye amejikita katika sheria za ajira. Alipata shahada yake ya sheria, katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Kabla ya kuwa katibu mkuu, Elizabethi amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho, ikiwamo afisa wa Idara ya Katiba na Sheria, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Naibu Katibu Mkuu (Bara).

Naye aliyekuwa mbunge wa Moshi Vijijini, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, Anthony Calist Komu, amechaguliwa kuwa naibu katibu mkuu mpya wa chama hicho, Tanzania Bara.

Komu, alikuwa mmoja wa wasisi wa NCCR – Mageuzi, amechukua nafasi hiyo, kutoka kwa Rehema Sam Kahangwa.

Mwanasiasa huyo machachari alijiunga na NCCR- Mageuzi, wakati kikiwa vuguvugu la kudai kuwapo mfumo wa vyama vingi nchini – The National Convention for Construction and Reform – mwaka 1990.

Wakati Komu anaendesha vuguvugu hilo, alikuwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mbunge wa Moshi Vijijini Anthony Komu

Mwingine aliyechaguliwa katika uongozi huo mpya, ni Suzana Maselle, ambaye alijiunga na chama hicho, kutokea Chadema, ambako alikuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri kati ya Novemba mwaka 2015 na Julai mwaka 2020.

Katika hatua nyingine, NCCR- Mageuzi kimerejesha upya mamlaka ya Kamati Kuu (CC), ambayo yalikuwa yameondolewa huko nyuma.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema, mabadiliko haya, tayasaidia sana chama hicho, kujisuka upya na kurejesha heshima yake ambayo ilitoweka kufuatia kuibuka kwa mgogoro mkubwa wa uongozi kati ya aliyekuwa mwenyekiti wake, Augustine Mrema na katibu mkuu wake, Mabere Marando.

Katika mgogoro huo, Mrema alidai kuwa Marando na Kamati Kuu (CC), wanataka kumuondoa kwenye kiti chake na hivyo akapendekeza kwa NEC, kumfukuza Marando, kuvunja CC na kuwafuta uwanachama viongozi wengine wandamizi, jaribio ambalo lilishindwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!