Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi amepelekwa hospitali akiugua maradhi ya kifua. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa iliyotolewa kwa umma na Msemaji wa Familia, Abdullah Ali Mwinyi imesema Mzee Mwinyi anaendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.
“Kutokana na ushauri wa madaktari wake, familia imeona ni vyema apate faragha akiwa anapatiwa matibabu.
“Hivyo Familia inaiomba jamii kumkumbuka kwenye Dua, Sala, na Maombi.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie shifaa ya haraka Mzee wetu pamoja na wagonjwa wengine wote wanaokabiliwa na maradhi mbali mbali,” amesema.
Leave a comment