Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwinyi amwombea msamaha Mkapa
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwinyi amwombea msamaha Mkapa

Spread the love

ALI Hassan Mwinyi, Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, amemwomba Mwenyezi Mungu kumsamehe Hayati Benjamin William Mkapa pale alipoteleza wakati wa uhai wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lupaso…(endelea).

Akizungumza baada ya kupewa nafasi hiyo na Rais John Magufuli wakati wa kutoa salamu za mwisho kijijini Lupaso, Mtwara, Mwinyi amesema, Mzee Mkapa naye ni mtu hivyo kuna mahali hukutenda aliteleza.

“Ndugu yetu marehemu Mkapa ni mwanadamu kama walivyo wengine, labda katika maisha yake aliwahi kufanya kosa asilolipenda muumba wetu.

“Katika hali kama hii, mwenzetu akiondoka, jambo la kwanza ni kumuombea usalama kwa Mwenyezi Mungu endapo kakosea. Kaanza kukosa baba yetu Bwana Adam, basi kama ana kosa, Mwenyezi Mungu amsamehe,” amesema.

Mwinyi ametoa pole kwa Mama Anna, Mjane wa Mkapa ndugu na jamaa kutokana na msiba huo, akisema miongoni mwa mambo anayokumbuka kutoka kwa Mzee Mkapa nikutokuwa na mchezo kazini.

Hata hivyo, Mzee Mwinyi amesema, kwenye shughuli hiyo kuna jambo amelikumbuka katika miaka ya nyuma, hata kama wengine wanaweza kuliona dogo.

“Mnaweza kuona ni jambo dogo, lakini kuna jambo ambalo nimeliona hapa. Nyinyi nyote mmevaa viatu, kwangu hili jambo si dogo.”

“Mimi nilivyaa viatu mara mbili, mara ya kwanza nilipokwenda jandoni nikiwa na miaka 13 na mara ya pili nilipovuna karafuu nikapata hela nikanunua viatu,” kauli hii ilimfanya Rais Magufuli na wengine kuangua kicheko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!