Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko MwanaHALISI yamalizana na JPM
Habari MchanganyikoTangulizi

MwanaHALISI yamalizana na JPM

Jabir Idrissa, Mhariri wa gazeti la MwanaHALISI
Spread the love

UONGOZI wa kampuni ya Hali Halisi Publishers Limited (HHPL), inayochapisha gazeti la MwanaHALISI, umemuomba radhi Rais Dk. John Magufuli, anaandika Faki Sosi.

Hatua hiyo imetekelezwa kupitia taarifa ya Mhariri wa MwanaHALISI, Jabir Idrissa, aliyoitoa kwa vyombo vya habari jana.

Katika taarifa hiyo, Idrissa alisema wamejikuta na wajibu wa kumtaka radhi Rais, Serikali anayoiongoza pamoja na umma wa Watanzania kutokana na usumbufu uliotokea.

Mhariri Idrissa amesema habari iliyochapishwa kwenye toleo la juzi Jumatatu, chini ya kichwa cha maneno, “Ufisadi ndani ya Ofisi ya JPM” haikuleta taswira nzuri kwa Rais Dk. Magufuli kwa kuwa imeonekana ni kama ufisadi umefanyika ndani ya ofisi yake ambayo ni Ikulu (State House).

Idrissa amesema baada ya kurudia kusoma kwa uangalifu habari husika, amejiridhisha kuwa tafsiri iliyoibuka kuwa Rais anahusika na ufisadi huo si sahihi na hivyo kuna haja ya kuweka sawa.

“Kwa hakika nimeridhika na wenzangu katika uongozi wa gazeti wamenielewa kuwa rais hahusiki kwa sababu ofisi ya Rais inaishia Ikulu na sio Idara nyingine ikiwemo Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitta (TAMISEMI),” amesema.

Alisema kwamba dhana kwamba Ikulu ni hata idara nyinginezo, haina usahihi kwa kuwa idara hizo zina mawaziri wake wanaozisimamia.

“Nimejirudi baada ya kufanya majadiliano marefu na Msajili wa Magazeti ambaye kwa kweli amenisaidia kuelewa kwa undani hisia zilizomjaa Rais kutokana na habari tuliyoichapisha. Tunamuomba radhi kwa hilo.

“Sasa kwa nafasi yangu ya Mhariri wa gazeti la MwanaHALISI, baada ya hatua ya kujirudi, niache akiba kwamba ni jukumu la serikali kuchukua hatua kwa kile tulichokusudia umma ukielewe ya kwamba hatua zichukuliwe dhidi ya ufisadi huo,” alisema Idrissa.

Juzi serikali kupitia Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dk. Hassan Abbas alitoa taarifa ya kumtaka Mhariri wa MwanaHALISI kumuomba radhi Rais kwa kosa la kumhusisha na ufisadi uliofanywa katika Shirika la Elimu Kibaha (SEK) tangu mwaka 2014.

Dk. Abbas alisema habari husika imejenga dhana kuwa Wizara ya Nchi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ambako shirika hilo linawajibika kiuongozi, inaihusu Ikulu wakati sivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!